Maumivu ya Kiungo: Viungo Vingi

Imepitiwa/Imerekebishwa Jun 2023

Viungo ni sehemu katika mwili wako ambapo mifupa miwili huungana, kama vile vifundo vya mikono, viwiko, mabega, nyonga, magoti na vifundo vya miguu.

Viungo pia vinapatikana sehemu ambazo huenda usifikirie, kama vile katikati ya mifupa mingi iliyo kwenye miguu, mikono, fupanyonga, na uti.

  • Maumivu makali kwa zaidi ya kiungo kimoja (aghalabu zaidi ya viungo 5) kwa kawaida yanasababishwa na tatizo la muda mrefu la viungo

  • Baadhi ya magonjwa yanayosababisha maumivu ya viungo yanaweza pia kusababisha upele, homa, maumivu ya macho, au vidonda mdomoni

Ni vitu gani husababisha maumivu kwenye viungo vingi?

Visababishi vya maumivu kwenye viungo vingi kwa kawaida ni tofauti na vile vya maumivu kwenye kiungo kimoja.

Maumivu kwenye viungo vingi husababishwa na:

  • Ugonjwa wa baridi yabisi

Ugonjwa wa baridi yabisi ni mwako wa viungo unaosababisha kuvimba, maumivu, na kukakamaa kwa viungo. Visababishi vya ugonjwa wa baridi yabisi ni tofauti kulingana na iwapo viungo vilianza kuumia ghafla (kwa muda mfupi) au umekuwa na maumivu kwa muda mrefu (ya kudumu).

Ugonjwa wa baridi yabisi unaotokea ghafla (kwa muda mfupi) katika zaidi ya kiungo kimoja mara nyingi husababishwa na:

Sababu zisizotokea sana ni pamoja na:

Ugonjwa wa baridi yabisi unaodumu kwa muda mrefu katika zaidi ya kiungo kimoja husababishwa na:

Matatizo yanayotokea sana nje ya viungo ambayo husababisha maumivu kwenye viungo ni pamoja na:

Je, ninapaswa kumwona daktari wakati gani kuhusiana na maumivu ya viungo vingi?

Mwone daktari mara moja ikiwa una maumivu kwenye zaidi ya kiungo kimoja na dalili yoyote ya tahadhari kati ya zifuatazo:

  • Wekundu, joto na kuvimba kwenye viungo

  • Upele mpya, madoa, au sehemu za zambarau kwenye ngozi

  • Vidonda kwenye mdomo, pua, au sehemu zako za siri

  • Maumivu ya kifua, kupumua kwa shida au kikohozi kipya au kikali

  • Maumivu tumboni mwako

  • Homa, kutokwa na jasho au mzizimo

  • Wekundu au maumivu ya macho

Mpigie daktari simu ikiwa una maumivu katika viungo vingi lakini huna dalili za tahadhari.

Je, nitarajie nini ninapokwenda kumwona daktari wangu?

Kabla ya kukupima, daktari wako atakuuliza kuhusu dalili zako na historia ya afya yako.

Dalili fulani zinaweza kumsaidia daktari kuamua kinachosababisha maumivu yako ya viungo. Dalili hizi ni pamoja na iwapo maumivu:

  • Yapo kwenye kiungo sawa cha pande zote mbili za mwili wako (kwa mfano, magoti yote mawili au mikono yote miwili)

  • Yanahama kutoka kiungo kimoja hadi kingine

  • Yapo kwenye uti wa mgongo na/au fupanyonga

Daktari anaweza kufanya vipimo kama vile:

  • Vipimo vya majimaji ya kiungo—madaktari hutoa majimaji kutoka kwenye kiungo chako kimoja kwa kutumia sindano kisha wanayatuma ili yakapimwe

  • Vipimo vya damu

  • Upimaji wa picha, kwa kawaida huwa eksirei, lakini wakati mwingine uchanganuzi wa CT (tomografia ya kompyuta) au MRI (upigaji picha kwa mvumo wa sumaku)

Madaktari wanatibu vipi maumivu kwenye viungo vingi?

Madaktari watatibu tatizo linalosababisha maumivu yako ya viungo. Kwa mfano, ikiwa una tatizo la kingamwili kwenda kinyume na mwili (wakati mfumo wa kinga wa mwili wako unasababisha mwili ushambulie tishu zake), huenda ukahitaji dawa za kutuliza mfumo wako wa kingamwili.

Madaktari wanaweza pia kukutibu maumivu ya viungo kwa:

  • Dawa za kupunguza uvimbe zisizo za steroidi (NSAID) au asetaminofeni

  • Kitambaa au kombeo

  • Kuwekelea kitu chenye joto au baridi

  • Matibabu ya kimwili

Mazoezi (kama vile kutembea au kuendesha baiskeli) husaidia kuhakikisha kuwa viungo havijakakamaa na kwamba misuli yako ina nguvu ikiwa una ugonjwa wa baridi yabisi uliodumu kwa muda mrefu.