Maumivu ya kichwa ni mojawapo ya sababu za kawaida za watu kwenda kwa daktari.
Mambo mengi yanaweza kusababisha maumivu ya kichwa ya kichwa
Maumivu mengi ya kichwa sio hatari. lakini mengine husababishwa na tatizo kubwa
Maumivu ya kichwa ya aina ya mkazo na kipandauso ni aina mbili ya maumivu ya kichwa yanayojulikana zaidi
Matatizo na sanasi yako, ubongo, au macho pia inaweza kusababisha maumivu ya kichwa
Mara nyingi, daktari anahitaji tu kukuchunguza, lakini wakati mwingine utahitaji vipimo kama vile uchanganuzi wa CT (tomografia ya Kompuyta) au kukinga majimaji ya uti wa mgongo
Je, maumivu ya kichwa husababishwa na nini?
Vyanzo vya kawaida vya maumivu ya kichwa ni:
Vyanzo vingine vya maumivu ya kichwa ni:
Maambukizi katika kichwa chako, kama vile homa ya uti wa mgongo, kuvimba kwa ubongo, au sinusitisi
Maambukizi ya mwili mzima kama vile ugonjwa wa Lyme, Homa ya madoadoa ya Rocky Mountain, au mafua
Kuvuja damu kwa ghafla katika ubongo wako (kuvuja damu ndani ya ubongo)
Kuepuka kafeini
Je, ninapaswa kuona daktari kwa maumivu ya kichwa wakati gani?
Muone daktari mara moja ikiwa unaumwa na kichwa na una mojawapo ya dalili zifuatazo za tahadhari:
Mabadiliko katika kuona kwako, udhaifu, kusinzia, kuchanganyikiwa, kutoweza kuwa wima, au kutatizika kuzungumza
Homa na shingo kukaza
Maumivu makali ya kichwa yanayotokea ghafla kama ngurumo
Maumivu pande za kichwa (kama unapochana nywele) au maumivu ya taya unapotafuna
Saratani, UKIMWI, au mfumo dhaifu wa kingamwili
Kuongezeka kwa maumivu ya kichwa
Macho kuwa mekundu na kuona vimulimuli ukiwa karibu na taa
Muone daktari ndani ya wiki moja ikiwa una:
Maumivu ya kichwa ambayo huanza baada ya kufikia miaka 50
Kupoteza wezo wa kuona
Kupungua uzani
Maumivu ya kichwa ambayo yanazidi kuongezeka au ya mara kwa mara
Ikiwa una umri wa zaidi ya miaka 50, maumivu yoyote mapya ya kichwa au mabadiliko ya maumivu ya zamani ya kichwa yanapaswa kuchunguzwa na daktari. Watu wazee wana uwezekano mkubwa wa kuwa na vyanzo vikubwa vya maumivu ya kichwa, na hata maumivu ya kichwa ya kawaida yanaweza kuwa vigumu zaidi kutibu kwa wazee.
Je, nitarajie nini ninapokwenda kumwona daktari wangu?
Daktari wako atakuuliza maswali kuhusu dalili zako na kukuchunguza. Daktari wako anaweza pia kufanya vipimo kama vile:
MRI (upigaji picha kwa mvumo wa sumaku) au uchanganuzi wa CT (tomografia ya kompyuta) wa kichwa chako
Kinga majimaji ya uti wa mgongo (kupenyeza sindano kwenye uti wa mgongo)
Je, madaktari hutibu vipi maumivu ya kichwa?
Matibabu yanategemea aina ya maumivu ya kichwa uliyo nayo:
Ikiwa tatizo lingine la kiafya linasababisha maumivu ya kichwa, madaktari watalitibu tatizo hilo
Kwa maumivu ya kichwa ya aina ya mkazo au maumivu ya kichwa yanayotokana na virusi, madaktari watakuagiza unywe dawa za maumivu kama vile aspirini, asetaminofeni, au ibuprofeni
Kwa kipandauso, madaktari watakupa dawa maalum