Muhtasari wa Uvimbe wa Ubongo

Imepitiwa/Imerekebishwa Dec 2022

Je, uvimbe wa ubongo ni nini?

Uvimbe wa ubongo ni sehemu iliyoota katika ubongo wako ambayo inaweza kuwa au isiwe saratani. Uvimbe wa ubongo unaweza kuanzia kwenye ubongo wako au unaweza kuwa umeenezwa kwenye ubongo wako (kueneza kansa) kutoka kwenye sehemu nyingine ya mwili wako.

  • Lakini uvimbe wa ubongo unaweza kusababisha matatizo makubwa hata ikiwa si wa saratani, kwa sababu fuvu lako ni gumu na hakuna uwazi wa uvimbe kuota

  • Jinsi uvimbe wa ubongo unavyoota, husukuma ubongo wako na kuongeza shinikizo ndani ya fuvu lako, hali ambayo inaweza kuathiri ubongo wako wote na kusababisha umauti kwa haraka

  • Uvimbe wa ubongo husababisha dalili mbalimbali kutegemea na sehemu ulipo katika ubongo wako

  • Dalili za kawaida hujumuisha kichwa kuuma, mabadiliko ya haiba ya mtu, kuyumba, shida ya umakinifu, kifafa, na udhaifu

  • Kwa watu wazima, dalili za uvimbe wa ubongo zinaweza kufananishwa kimakosa na tatizo la akili

  • Matibabu yanaweza kujumuisha upasuaji, tiba ya mionzi au tibakemikali

Zipi ni dalili za uvimbe wa ubongo?

Dalili za uvimbe wa ubongo zinaweza kuanza kwa ghafla au kuongezeka taratibu kwa muda mrefu. Dalili zinajumuisha:

  • Maumivu ya kichwa, hasa ikiwa yanatokea mara kwa mara au kuwa makali pale unapolala chini

  • Matatizo ya utendakazi wa akili na hali, kama vile kujitenga, kukasirika kila mara, kusinzia kila mara, au kuchanganyikiwa, au hali ya kufanya matendo ambayo ni tofauti na haiba yako ya kawaida

  • Kuhisi mgonjwa tumboni na kutapika

  • Uoni hafifu

  • Kizunguzungu, kuyumba, na udhaifu

  • Vifafa

  • Kuhisi hali ya usingizi na kuchanganyikiwa

Kwa kutegemea sehemu yenye uvimbe katika ubongo, unaweza kuathiri:

  • Mwendo katika mkono, mguu, au upande mmoja wa mwili wako

  • Kuzungumza au kuelewa lugha

  • Uwezo wako wa kusikia, kunusa, au kuona

Je, madaktari wanawezaje kujua kuwa nina uvimbe wa ubongo?

Madaktari hufanya vipimo kama vile:

Wakati mwingine madaktari wanaweza kugundua ni uvimbe wa aina gani kupitia MRI au uchanganuzi wa CT Wakati mwingine madaktari hufanya biopsi ya uvimbe (uondoaji wa kipande cha tishu kwa uchunguzi kwenye hadubini).

Je, madaktari wanatibu vipi uvimbe wa ubongo?

Madaktari hutibu uvimbe wa ubongo kwa kutegemea sehemu ulipo na dalili ulizonazo. Tofauti na uvimbe mwingine unaopatikana katika sehemu nyingine za mwili, haijalishi kama uvimbe wa ubongo ni wa saratani au si wa saratani. Uvimbe usio wa kansa unaweza pia kusababisha matatizo makubwa ya ubongo. Matibabu yanajumuisha:

Ikiwa una uvimbe mdogo sana, usio wa kansa ambao hausababishi dalili nyingi, madaktari wanaweza kuuacha.

Masuala ya mwisho wa uhai

Watu ambao wana uvimbe wa ubongo wenye saratani kwa haraka sana wanaweza kushindwa kufanya maamuzi yanayohusu huduma zao za matibabu na mahitaji yao ya masula ya kipindi cha mwisho cha uhai wao. Ikiwa una uvimbe wowote wa ubongo wenye saratani, zungumza na mshauri au mtoa huduma za jamii ili akusaidie kutengeneza maelekezo ya mapema. Maelekezo ya mapema ni mpango wa kuwafahamisha wapendwa wako na madaktari ni huduma gani za matibabu ambazo unazihitaji wakati ukielekea mwisho wa uhai wako.