Tibakemikali ni nini?
Tibakemikali ni dawa inayoharibu seli za saratani. Tibakemikali hufanya kazi kwa kuzuia ukuaji wa seli. Lakini kwa kuwa seli zote za mwili hukua, dawa za tibakemikali huharibu pia baadhi ya seli za kawaida na kusababisha madhara. Si dawa zote zinazotibu saratani huchukuliwa kama tibakemikali, kwa mfano, tiba ya mfumo wa kinga ni tofauti.
Tibakemikali haifanyi kazi kwenye kansa zote
Kuna aina nyingi za dawa za tibakemikali—dawa utakayopata inategemea aina ya saratani uliyo nayo
Dawa nyingi za tibakemikali hutolewa kupitia mshipa wako (IV)
Madaktari wanaweza kukupa dawa kadhaa za tibakemikali kwa wakati mmoja au wanaweza kuunganisha tibakemikali na aina nyinginezo za matibabu ya saratani, kama vile upasuaji au tiba ya mionzi
Madaktari wanaweza kukupa dawa nyinginezo ili kupunguza athari za tibakemikali
Wakati mwingine baada ya kutumia dawa ya tibakemikali kwa muda, seli za kansa huanza kukinza dawa hiyo. Tibakemikali huacha kuziua. Hali hii inapotokea, daktari wako anaweza kujaribu dawa tofauti.
Je, athari mbaya za tibakemikali ni zipi?
Tibakemikali ina sifa za kusababisha athari mbaya na wakati mwingine athari hatarishi. Dawa mpya za tibakemikali zina madhara machache kuliko za zamani. Na madaktari sasa wana matibabu bora ya baadhi ya madhara yanayotokea.
Athari mbaya zinazotokea sana ni:
Kuhisi mgonjwa kwenye tumbo lako au kutapika
Kutohisi njaa kama kawaida
Kupungua uzani
Kuhisi udhaifu na uchovu
Kuharisha (kutokwa kinyesi chepesi chenye umajimaji na kinachotoka mara kwa mara)
Kupoteza nywele zako
Vidonda kwenye kinywa au pua
Tibakemikali mara nyingi huathiri seli nzuri zinazotengeneza damu kwenye uboho. Hali hii inaweza kupunguza idadi ya seli zako za damu, jambo ambalo linaweza kusababisha:
Kiwango cha chini cha damu (anemia), iwapo idadi ya seli zako nyekundu za damu imepungua
Maambukizi mabaya, iwapo idadi ya seli zako nyeupe imepungua
Kuvuja damu, iwapo idadi ya chembe sahani imepungua
Anemia inaweza kusababisha:
Udhaifu
Kuhisi kizunguzungu
Kupumua kwa shida au maumivu ya kifua
Maambukizi kutokana na idadi iliiyopungua ya seli nyeupe yanaweza kusababisha:
Homa
Idadi iliyopungua ya chembe sahani inaweza kusababisha:
Kuvimba kwa urahisi
Kuvuja damu kutoka puani, fizi, au rektamu
Tibakemikali inaweza pia kuathiri ogani nyinginezo kando na uboho na kusababisha matatizo mengine ya kimatibabu:
Uharibifu kwenye mapafu, moyo, au ini
Ugumba (matatizo ya kupata ujauzito)
Wakati mwingine uwezekano mkubwa wa kupata kansa nyingine kama vile lukemia