Kipandauso

Imepitiwa/Imerekebishwa Sept 2024

Je, kipandauso ni nini?

Kipandauso sio maumivu mabaya ya kichwa tu. Kipandauso ni aina fulani ya maumivu mabaya ya kichwa. Maumivu yanaweza kuwa kwenyeupande mmoja au pande zote mbili za kichwa chako. Unaweza kujihisi mgonjwa kwa tumbo lako, kutapika, na kuwa na hisia kali zaidi kwa mwanga, sauti, na harufu.

  • Kipandauso kwa kawaida hutokea katika kipindi cha masaa 4 hadi siku kadhaa

  • Kipandauso huja na kutoweka na inaweza kutokea mara moja tu kwa muda au mara nyingi kwa mwezi

  • Kipandauso mara nyingi huanza wakati wa kubalehe au unapokuwa mtu mzima, na hutokea kidogo unapokuwa na zaidi ya miaka 50

  • Kipandauso ni hutokea zaidi kwa wanawake

  • Unaweza kuwa na uwezo wa kujua mambo ambayo hukufanya wewe kuwa na kipandauso (kama vile mvinyo mwekundu) na kuyaepuka

  • Madaktari hawawezi kuponya kipandauso, lakini watakupa dawa ili kupunguza dalili

Je, kipandauso husababishwa na?

Unapata kipandauso wakati seli za neva na mishipa ya damu kwenye ubongo wako huchochewa na kusumbuliwa. Madaktari hawana uhakika kwa nini hili hutokea kwa baadhi ya watu na si kwa wengine. Hata hivyo, kipandauso inaonekana kuwa hali ya kurithi. Kwa hivyo ikiwa una wanafamilia wanaopata kipandauso, kuna uwezekano mkubwa wa kuipata.

Je, ni nini huchochea kipandauso?

Kwa watu wanaopata kipandauso, mambo fulani yanaweza huchochea hali hiyo:

  • Viwango vya juu vya homoni ya kike ya estrojeni—ambayo hutokea hasa wakati wa kubalehe, kabla, wakati, na baada ya hedhi ya mwanamke, baada ya kujifungua, mwanzoni mwa ukomo wa hedhi, au wakati wa kutumia tembe za kudhibiti uzazi (zilizo na estrojeni)

  • Msisimko mwingi wa hisi zako, kama vile taa zinazomulika au harufu kali

  • Msongo wa mawazo

  • Usingizi usiotosha

  • Mabadiliko ya hali ya hewa

  • Mvinyo mwekundu

  • Njaa, haswa kutokana na kuruka milo

Je, dalili za kipandauso ni zipi?

Una maumivu kichwani. Mara nyingi maumivu yanagonga au kupiga na upande mmoja tu. Lakini maumivu yanaweza pia kuwa ya dhabiti au kwa pande zote mbili. Pia utakuwa na dalili zingine kama vile:

  • Maumivu ya kichwa huwa mabaya zaidi kukiwa na mwanga unaosogea, mwanga mkali, sauti kubwa, na harufu kali

  • Kuhisi mgonjwa kwenye tumbo lako au kutapika

  • Una tatizo la kuwa makini

Kipandauso sio hatari. Hata hivyo, kipandauso hakipendezi. Watu wengi hawawezi kufanya shughuli zao za kawaida wakati wana kipandauso. Watu wengi hulazimika kulala kwenye chumba chenye giza hadi kipandauso kitoweke.

Dalili za kutahadharisha ukiwa na kipandauso

Unaweza kuwa na dalili za mapema kabla ya kupata maumivu ya kichwa:

  • Kutohisi njaa kama kawaida

  • Kuhisi mgonjwa tumboni

  • Mabadiliko ya hisia

Takriban mtu 1 kati ya 4 walio na kipandauso huwa na mabadiliko katika uwezo wao wa kuona, usemi, au mienendo kabla tu ya maumivu ya kichwa kuanza. Hii inaitwa aura. Watu wengine hupata aura lakini hawana maumivu ya kichwa, au maumivu kidogo tu ya kichwa. Dalili za aura zinaweza kujumuisha:

  • Kuona taa zinazomulika au sehemu isiyoonekana iliyo na kingo zinazopepea (aura inayojulikana zaidi)

  • Hisia za kuwashwa ambazo husafiri kwa mkono wa mtu

  • Kuyumbayumba

  • Udhaifu katika mkono au mguu

  • shida ya kuzungumza

Je, madaktari wanawezaje kujua kuwa nina kipandauso?

Madaktari anaweza kubainisha kulingana na dalili zako na kwa kufanya uchunguzi.

Unapoanza kupata kipandauso, madaktari wanaweza kukufanyia vipimo vingine, kama vile MRI (upigaji picha kwa mvumo wa sumaku) ya kichwa chako, ili kuona ikiwa tatizo lingine linasababusha uwe na maumivu ya kichwa.

Mara tu madaktari wanapojua una kipandauso, wanafanya vipimo ikiwa tu maumivu ya kichwa ni tofauti na kipandauso chako cha kawaida. Aina tofauti za maumivu ya kichwa yanaweza kumaanisha kuwa una tatizo tofauti.

Je, madaktari hutibu vipi kipandauso?

Ikiwa una kipandauso kidogo hadi cha wastani, madaktari watakuagiza umeze:

  • Dawa ya maumivu, kama vile asetaminofeni, ibuprofeni, au aspirini

  • Dawa zinazoondoa kichefuchefu, zinazoweza kutibu kichefuchefu na maumivu ya kichwa

Madaktari wanaweza kukuambia ujilaze kwenye chumba chenye giza, tulivu na ujaribu kulala. Kipandauso mara nyingi hutoweka wakati wa kulala.

Ikiwa una kipandauso kikali madaktari wanaweza kukupa:

  • Dawa zinazoitwa triptani, ambazo hufanya kazi vizuri zaidi zinapomezwa mara moja

  • Dawa za kichefuchefu zinazotolewa kupitia mshipa wa damu (baadhi ya dawa huondoa kichefuchefu na maumivu ya kichwa)

  • Majimaji kupitia kwenye mshipa ikiwa umepungukiwa na maji mwilini (huna maji ya kutosha mwilini mwako) kutokana na kutapika

Ikiwa unapata kipandauso cha mara kwa mara, madaktari wanaweza kukuomba uweke shajara ya maumivu ya kichwa ili uandike chini unapokuwa na kipandauso, chanzo chake, na matibabu yako, ili uweze kutafuta mielekeo.

Je, ninawezaje kuzuia kipandauso?

Madaktari wanaweza kukupa dawa ya kuzuia kipandauso ikiwa una:

  • Kipandauso ambacho hutokea mara kwa mara na huwa hakipunguzwi maumivu kwa dawa zingine za maumivu

  • Kipandauso kikali sana ambacho kinakuzuia kufanya shughuli zako za kila siku

Mambo mengine ambayo yanaweza kusaidia:

  • Shughuli za kukusaidia kupumzika na kupunguza msongo wa mawazo

  • Kuepuka vitu vinavyosababisha kipandauso chako