Saratani ya Kongosho

Imepitiwa/Imerekebishwa Jan 2023

Kongosho lako ni kiungo kilicho upande wa juu wa tumbo lako ambacho hutengeneza juisi za mmeng'enyo. Kongosho lako pia hutoa insulini na homoni nyingine ambazo husaidia kudhibiti sukari kwenye damu.

Kutambua Kongosho Ilipo

Je, saratani ya kongosho ni nini?

Saratani ni ukuaji wa seli mwilini kwa namna isiyoweza kudhibitiwa. Seli ni elementi ndogo zinazoshikamana kuunda viungo vya mwili wako. Seli zina majukumu maalum. Viungo tofauti vimeundwa na aina tofauti za seli. Aina yoyote ya seli inaweza kuwa yenye saratani. 

Saratani ya kongosho ni saratani ambayo huanzia kwenye kongosho lako.

  • Dalili hujumuisha maumivu ya tumbo, kupungua uzani na kutapika

  • Mara nyingi saratani ya kongosho husambaa kabla ya kutambulika

  • Upasuaji unaweza kuponya saratani ya damu kabla haijasambaa

  • Mara baada ya kusambaa kwa saratani ya kongosho, ni nadra sana kupona

Je, nini husababisha saratani ya kongosho?

Una uwezekano mkubwa wa kupata saratani ya kongosho ikiwa:

  • Kuvuta sigara

  • Una ugonjwa sugu wa kuvimba kwa kongosho

  • Una wanafamilia wenye saratani ya kongosho

  • Wewe ni Mwafrika

  • We ni mwanaume

Dalili za saratani ya kongosho ni zipi?

Kwa kawaida saratani ya kongosho haisababishi dalili hadi inapokuwa imesambaa. Kisha, dalili zako zinaweza kujumuisha:

  • Maumivu makali ya sehemu ya juu ya tumbo, ambayo pia unaweza kuyahisi katika sehemu ya kati ya mgongo wako—unaweza kuhisi afadhali unapoinama kwa mbele au kujikunja

  • Kupungua uzani

  • Homa ya nyongo ya manjano (ngozi na weupe wa macho kuwa manjano)

  • Kuvimba tumbo au kuhara

Watu wengi wenye saratani ya kongosho pia wana kisukari kwa sababu kongosho haliwezi kuzalisha insulini ya kutosha.

Madaktari wanawezaje kujua kama nina saratani ya kongosho?

Madaktari hutafuta uwepo wa saratani ya kongosho kwa kutumia:

Je, madaktari hutibu vipi saratani ya kongosho?

Ikiwa madaktari hawadhani kuwa saratani imesambaa, wanaweza kufanya:

Ikiwa saratani tayari imesambaa, upasuaji hausaidii. Ikiwa ilisambaa tu kwenye tishu za karibu, madaktari wanaweza kukupatia tibakemikali na tiba ya mionzi. Ikiwa saratani imesambaa sehemu kubwa, madaktari watatibu dalili zako ili kujaribu kukufanya ujisikie afadhali zaidi. Matibabu ya dalili ni pamoja na:

  • Dawa za maumivu au sindano

  • Vimeng'enya vikichukua nafasi ya juisi za mmeng'enyo

  • Insulini iwapo utapata kisukari