Paiodema Gangrenosam

Imepitiwa/Imerekebishwa Jan 2023

Paiodema gangrenosam ni nini?

Paiodema gangrenosam ni ugonjwa wa ngozi ambapo unapata majeraha makubwa kwenye ngozi yako, hasa kwenye miguu.

  • Huwapata hasa watu wenye umri kuanzia miaka 25 hadi 55

  • Madaktari hawajui chanzo chake ni nini, lakini mara nyingi huwapata watu ambao wana matatizo mengine ya kiafya, kama vile ugonjwa wa uchochezi wa matumbo

  • Wakati mwingine hutokea kwa ngozi iliyojeruhiwa hivi karibuni

  • Unapata viuvimbe au malengelenge madogo madogo ambayo hugeuka na kuwa vidonda vilivyo wazi

  • Matibabu yake hujumuisha kufunga vidonda, malai, na dawa

Je, nini husababisha paiodema gangrenosam?

Madaktari hawajui nini hasa husababisha paiodema gangrenosam, lakini wanadhani ni tatizo linalohusiana na mfumo wa kingamwili. Paiodema gangrenosam huwapata sana watu ambao wana matatizo fulani ya kiafya, kama vile:

Zipi ni dalili za paiodema gangrenosam?

Dalili za paiodema gangrenosam ni pamoja na:

  • Uvimbe au malengelenge mekundu ambayo hugeuka na kuwa jeraha lililo wazi, lenye uchungu ambalo hukua kwa haraka

  • Eneo lililoinuliwa kuzunguka jeraha ambalo ni jeusi au la zambarau

  • Homa

  • Hisia ya jumla ya kuumwa

Majeraha yatokanayo na paiodema gangrenosam yanaweza kuwa mabaya zaidi kutokana na:

  • Bayopsi (uondoaji wa kipande cha tishu kwa uchunguzi)

  • Kusafisha seli zilizokufa kutoka kwenye kidonda (inaitwa debridement)—japokuwa uondoaji wa seli zilizokufa husaidia kidonda kupona, kuondoa seli zilizokufa kwenye majeraha ya paiodema gangrenosam huyafanya yawe na hali mbaya zaidi badala ya kupata ahueni

Mara nyingine dalili zinaweza kusambaa katika maeneo mengine, kama vile eneo la tumboni, mifupa, mapafu, au misuli.

Madaktari wanawezaje kujua ikiwa nina paiodema gangrenosam?

Mara nyingi madaktari wanaweza kufahamu ikiwa una paiodema gangrenosam kwa kutazama majeraha.

Je, madaktari hutibu vipi paiodema gangrenosam?

Madaktari hutibu paiodema gangrenosam kwa kutumia:

  • Kufunga vidonda ili kulinda ngozi yako

  • Kotikosteroidi

  • Mara nyingine dawa ya kutuliza mfumo wa kingamwili wako

Mara nyingi madaktari hawafanyi upasuaji, kwa sababu kufanya hivyo hufanya majeraha kuwa mabaya zaidi.