Kaboni Monoksidi ni gesi isiyo na rangi, isiyo na harufu na isiyo na ladha. Inazalishwa kutoka kwa vitu vinavyochemeka, ikiwa ni pamoja na injini za magari, mifumo ya joto na moto ya kuni.
Je, athari ya sumu ya kaboni Monoksidi ni nini?
Sumu ya kaboni monoksidi ni maradhi yanayotokana na kuvuta hewa yenye kiasi kikubwa cha kaboni monoksidi. Kaboni monoksidi inaweza kukudhuru kwa sababu inazuia oksijeni iliyo kwenye damu kufikia seli zako.
Watu wanaovuta hewa yenye kiasi kikubwa cha kaboni monoksidi wanaweza kuaga dunia.
Dalili ni pamoja na kuumwa na kichwa, kuhisi mgonjwa tumboni, kuchanganyikiwa, kutofanya mambo ipasavyo (uratibu mbaya), na uchovu
Unaweza kufikiria kimakosa kuwa una homa au ugonjwa mwingine
Sakinisha vifaa vya kugundua kaboni monoksidi nyumbani mwako—vinakutahadharisha ikiwa kuna kaboni monoksidi kwenye hewa
.Ikiwa unafikiri kuwa unaweza kuwa unavuta hewa ya kaboni monoksidi, nenda nje ili upate hewa safi mara moja, na upige simu kwa usaidizi wa dharura wa matibabu (911 katika maeneo mengi nchini Marekani).
Je, chanzo cha athari ya sumu ya kaboni monoksidi ni nini?
kaboni monoksidi hutokana na kuchoma vitu. Chochote kinachohusisha kuchoma kitu kinaweza kuleta kaboni monoksidi: nyumba kuchomeka, injini za magari, moto wa kuni, tanuru, hita za gesi, hita za mafuta ya taa na stovu. Ili kuzuia sumu ya kaboni monoksidi, moshi lazima uvukuliwe (kuachiliwa nje) ipasavyo.
Je, dalili za athari ya sumu ya kaboni monoksidi ni zipi?
Dalili za kwanza ni:
Maumivu ya kichwa au kizunguzungu
Kuhisi mgonjwa tumboni
Kutapika
Kuhisi uchovu au kuwa na tatizo la kuwa makini
Kutekeleza mambo ovyo (kuchanganyikiwa)
Baadaye, au kwa sumu kali zaidi ya kaboni monoksidi, unaweza
Kuchanganyikiwa
Kupoteza fahamu au kutoitika
Kuwa na matukio ya kifafa (wakati mwili wako unasonga na kutetemeka ghafla bila udhibiti wako)
Kuwa na maumivu katika kifua chako
Kuhisi kama huwezi kupumua
Kujihisi dhaifu au mnyonge
Sumu kali inaweza kukuua.
Je, madaktari wanawezaje kujua kama nina athari ya sumu ya kaboni monoksidi?
Madaktari watachukua sampuli ya damu yako ili kuchunguza kama ina kaboni monoksidi.
Je, madaktari humtibu mgonjwa aliyeathirika na sumu ya kaboni monoksidi vipi?
Madaktari watakupa oksijeni. Oksijeni hiyo itasaidia kuondoa kaboni monoksidi kutoka kwa damu yako.
Ikiwa una kiasi kidogo cha sumu, utahitaji tu hewa safi
Ikiwa una sumu kali, unaweza kuhitaji kupumua oksijeni kupitia kwa barakoa ya uso
Je, ninawezaje kuzuia kupata sumu ya kaboni monoksidi?
Sakinisha kifaa cha kugundua kaboni monoksidi nyumbani kwako
Hakikisha moto wa kuni, tanuru, na stovu zote zimewekwa na kuvukuzwa kwa usahihi
Usiwashe gari lako kwenye gareji iliyofungwa