Je, Vipele vya sehemu za siri vya ujauzito (Pemphigoid gestationis) ni nini?
© Springer Science+Business Media
Pemphigoid gestationis ni vipele vya nadra, vinavyowasha sana ambavyo hutokea tu unapokuwa mjamzito, kwa kawaida katika miezi mitatu ya 2 au 3 ya ujauzito.
Vipele mara nyingi huanza karibu na kitovu chako na huonekana kama madoa mekundu yaliyoinuka
Baadaye, vipele huenea na kugeuka kuwa malengelenge yenye umbo lisilo la kawaida, yaliyojaa majimaji
Vipele huwa na hali mbaya zaidi mara tu baada ya kujifungua na hupotea ndani ya wiki au miezi michache
Ikiwa una vipele, mtoto wako anaweza kuzaliwa na vipele, lakini kwa kawaida huisha bila tiba
Mara tu unapokuwa na pemphigoid gestationis, kuna uwezekano mkubwa wa kuwa nayo katika ujauzito mwingine wa siku zijazo
Je, ni nini husababisha pemphigoid gestationis?
Madaktari wanafikiria kuwa pemfigoidi gestationisi ni mmenyuko wa kingamwili. Mmenyuko wa mfumo wa kingamwili kwenda kinyume na mwili wako ni wakati mfumo wa kinga unaposhambulia mwili wako.
Je, madaktari wanawezaje kujua ikiwa nina pemphigoidi gestationis?
Kwa kawaida madaktari wanaweza kujua kwa kuangalia tu vipele vyako
Wanaweza kufanya pia vipimo vya ngozi na vipimo vingine ili kumchunguza mtoto wako
Je, madaktari hutibuje pemphigoid gestationis?
Kwa kawaida kwa kutumia krimu ya kotikosteroidi ambayo unapaka kwenye ngozi yako ili kusaidia isiwashe sana
Ikiwa vpele vyako vitaenea sana, unaweza kupata kidonge chenye kotikosteroidi, kama vile prednisone