Kandidiasi (Maambukizi ya Chachu)

Imepitiwa/Imerekebishwa Oct 2024

Nyenzo za Mada

kandidiasisi ni nini?

Kandidiasi ni maambukizi yanayosababishwa na Chachu ya Kandida. Kwa sababu chachu ni aina ya kuvu, kandidiasi ni maambukizi ya kuvu, lakini mara nyingi huitwa maambukizi ya chachu. Chachu ya Kandida mara nyingi huishi kwenye mwili wako kwa kiasi kidogo pasipo kuonyesha dalili zozote. Lakini wakati mwingine zinaweza kukua kupita kiasi au maambukizi yanaweza kutokea.

  • Maambukizi ya chachu mara nyingi hutokea kwenye sehemu ya juu ya mwili wako, ikiwemo ngozi, mdomo, au uke wako

  • Wakati mwingine watu wenye mfumo wa kingamwili ambao ni dhaifu hupata maambukizi ya chachu kwenye ogani zao za ndani (kandidiasi inayoenea kwa hatua), hali ambayo inaweza kutishia maisha

  • Maambukizi ya chachu yanaweza kusababisha wekundu, upele, kuwasha/mwasho, kuvimba, au madoa meupe yenye rangi ya malai

  • Baadhi ya upele utokanao na nepi husababishwa na maambukizi ya chachu

  • Madaktari hutibu maambukizi ya chachu kwa kutumia malai au dawa za kumeza

Je, nini husababisha maambukizi ya chachu?

Maambukizi ya chachu husababishwa na chachu ya Kandida, kuvu ambayo kwa kawaida huishi mwilini mwako kwa kiasi kidogo. Ikiwa katika kiasi kidogo, huwezi kuitambua. Ikiwa chachu itaongezeka kwa kiasi kikubwa, unapata kipele.

Baadhi ya sababu za chachu kuongezeka kwa kiasi kikubwa hujumuisha:

  • Kuvaa nguo za ndani zenye kubana, sidiria, au nguo nyingine ambazo huweka jasho karibu na mwili wako

  • Kuwaacha watoto wachanga wakiwa na nepi zilizolowa au chafu kwa muda mrefu

  • Kuwa na kisukari

  • Kuwa na mfumo wa kingamwili ambao ni dhaifu kwa sababu ya matatizo kama vile maambukizi ya Virusi Vya Ukimwi au saratani

  • Kutumia dawa za kuua bakteria

Chachu hupenda kuishi gizani, kwenye maeneo yenye unyevunyevu mwilini mwako Hivyo, maambukizi ya chachu hutokea sana katika maeneo haya:

  • Chini ya mikunjo ya ngozi kwa watu ambao ni wanene sana

  • Mdomoni

  • Chini ya matiti ya wanawake

  • Kwenye eneo la kinena au uke

Zipi ni dalili za maambukizi ya chachu?

Dalili hutegemea eneo lenye maambukizi ya chachu:

  • Kwenye ngozi yako: Upele mbichi, wenye wekundu wa kung'aa

  • Ndani ya uke wako: Madoa meupe na vitu vyeupe mfano wa jibini kutoka ukeni

  • Mdomoni mwako: Madoa meupe (kuvimba ndani kwa ndani)

  • Kwenye pembe ya mdomo wako: Mpasuko kwenye ngozi

Maambukizi ya Chachu
Thrush
Thrush

Creamy white patches are seen inside the mouth and may bleed when scraped off. This finding is typical of thrush, which is caused by infection with Candida.

... soma zaidi

Image provided by Thomas Habif, MD.

Angular Cheilitis
Angular Cheilitis

This photo shows angular cheilitis (sometimes called perlèche) caused by Candida infection at the corners of the mouth.

© Springer Science+Business Media

Nail Infection (Candidiasis)
Nail Infection (Candidiasis)

Nail infections caused by Candida can affect the nail plate (onychomycosis—seen at the bottom of the nail), the edges of the nail (paronychia), or both.

... soma zaidi

Image courtesy of CDC/Sherry Brinkman via the Public Health Image Library of the Centers for Disease Control and Prevention.

Diaper Rash Caused by Candida
Diaper Rash Caused by Candida

This photo shows a rash caused by the yeast Candida.

Image provided by Thomas Habif, MD.

Vaginal Candidiasis
Vaginal Candidiasis

This photo shows swelling and redness of the vagina and a white discharge caused by a yeast infection.

BIOPHOTO ASSOCIATES/SCIENCE PHOTO LIBRARY

Madaktari wanawezaje kujua ikiwa nina maambukizi ya chachu?

Madaktari kwa kawaida wanaweza kujua ikiwa una maambukizi ya kuvu kwa kuiangalia tu. Ili kufahamu kwa hakika, daktari anaweza kubandua sehemu ndogo sana ili kuitazama kwenye hadubini.

Je, maambukizi ya kuvu hutibiwa vipi?

Matibabu hutegemea mahali yalipo maambukizi ya chachu.

Kwa maambukizi ya kwenye ngozi yako, madaktari watakufanya:

  • Upake malai, poda, au bidhaa nyingine zenye dawa ya kuua kuvu kwenye eneo lenye maambukizi

  • Uweka ngozi yako katika hali ya ukavu (kwa mfano, kwa kubadilisha nepi za mtoto mchanga kila mara)

  • Utumie dawa za kumeza, ikiwa maambukizi ni makali

Kwa maambukizi ya chachu kwenye uke wako, madaktari watakufanya:

  • Upake malai ya dawa ya kuvu ndani na nje ya uke wako

  • Wakati mwingine, umeze dawa

Kwa uvimbe wa ndani kwa ndani kwa watu wazima, madaktari watakufanya:

  • Utumie dawa ya kuvu

  • Wakati mwingine, usukutue kwa dawa ya kuvu ya kiowevu (nystatin)

Kwa uvimbe wa ndani kwa ndani kwa watoto wachanga, madaktari watakufanya upake dawa ya kuvu ya kiowevu mdomoni mwa mtoto wako mchanga.