Mwasho wa jock

(Tinea wa Kinena)

Imepitiwa/Imerekebishwa Oct 2022

Mwasho wa kinena ni nini?

Mwasho wa kinena ni kipele cha mwasho kinachotokea kwenye eneo la kinena (msamba) Ni maambukizi ya kuvu ambayo hutokea kwenye maeneo yenye hali ya uvuguvugu na unyevunyevu

Una uwezekano mkubwa wa kupata mwasho wa kinena ikiwa:

  • Wewe ni mwanamume, kwasababu unyevunyevu hunasa katikati ya korodani na mapaja

  • Hali ya hewa ni ya uvuguvugu

  • Unavaa nguo mbichi na zenye kubana

  • Una uzani mkubwa kupita kiasi na una mikunjo kwenye ngozi

Zipi ni dalili za mwasho wa kinena?

Dalili zinajumuisha:

  • Upele mwekundu wenye kuwasha kwenye kinena na wakati mwingine kwenye eneo la juu la mapaja

  • Upele unaweza kuwa na ukingo wa rangi ya waridi wenye magamba

  • Hali mbaya ya mwasho wa kinena inaweza kusababisha maumivu

Madaktari wanawezaje kujua ikiwa nina maambukizi ya mwasho wa kinena?

Mara nyingi madaktari wanaweza kufahamu kuwa ni mwasho wa kinena kwa kuutazama tu. Mara chache, madaktari wanaweza kukwangua kipande kidogo cha ngozi yako ili kukichunguza kwenye hadubini.

Je, madaktari wanatibu vipi mwasho wa kinena?

Madaktari hutibu mwasho wa kinena kwa kutumia:

  • Malai ya dawa ya kuvu ya kupaka kwenye ngozi

  • Wakati mwingine, dawa za kumeza

Mara nyingi maambukizi haya hurejea kwa zaidi ya mara moja, hasa ikiwa pia una maambukizi ya kuvu kwenye miguu au kucha za vidole vya miguu (tinea ya mguu), kwa sababu kuvu linaweza kusambaa kutoka maeneo hayo hadi kwenye kinena chako.