Magonjwa ya paraneoplastiki

Imepitiwa/Imerekebishwa Jul 2023

Tatizo linaloambatana na saratani ni nini?

Neoplasm ni uvimbe usio wa kawaida katika mwili wako ambao unaweza kuwa na seli za saratani. Ikiwa kitu kinarejelewa kama “neoplastiki,” basi kinahusiana na uvimbe huo. Matatizo ya paraneoplastiki ni mkusanyiko wa dalili zinazosababishwa na saratani. Dalili hizo hutokea katika sehemu tofauti ya mwili wako kando na mahali saratani ilipo.

Watu wengi walio na saratani huwa hawapati tatizo la paraneoplastiki.

  • Magonjwa ya paraneoplastiki husababishwa na saratani yako kutengeneza homoni au mfumo wako wa kingamwili kutengeneza seli za kingamwili zinazoshambulia tishu za mwili wako (ziitwazo kingamwili otomatiki) zinazosafirishwa na damu yako

  • Magonjwa ya paraneoplastiki husababisha dalili tofauti kulingana na tishu na ogani zilizoathiriwa

  • Angalau mtu 1 kati ya watu 5 walio na saratani hupata magonjwa ya paraneoplastiki—mara nyingi hutokea kwa wagonjwa wa saratani ya mapafu

Je, ni zipi dalili za magonjwa ya paraneoplastiki?

Dalili za jumla

  • Homa

  • Kutokwa jasho usiku

  • Kupoteza hamu ya kula

  • Kupungua uzani

Dalili za ngozi

  • Kuwasha

  • Kuiva uso, kunakosababisha uso, shingo, au sehemu ya juu ya kifua kuwa na joto kiasi na kuwa rangi nyekundu

Dalili za kinyurolojia (ubongo, uti wa mgongo, na neva)

  • Udhaifu au kuishiwa na nguvu

  • Kupoteza uwezo wa kuhisi

  • Kutekeleza polepole

  • Matatizo ya kutumia sehemu mbalimbali za mwili jinsi unavyotaka, kama vile mikono au miguu

  • Shida ya kuzungumza

  • Kizunguzungu

  • Kuona vitu viwili viwili (unapoona vitu 2 badala ya kimoja) au kushindwa kudhibiti mwendo wa macho yako

Saratani inaweza kusababisha dalili hizi bila kubana neva au uti wako wa mgongo.

Dalili za endokrini (mfumo wa homoni)

  • Udhaifu

  • Kuongeza uzani

  • Shinikizo la juu la damu au matatizo ya vali ya moyo

  • Kuchanganyikiwa

  • Matatizo ya figo

  • Ngozi nyekundu na yenye joto

  • Kuforota

  • Kuharisha

Dalili nyinginezo

  • Kuvimba misuli kunakosababisha udhaifu na kuumwa

  • Kuvimba viungo kwenye maumivu kunakoweza kubadilisha umbo la vidole vya mikono na miguu

  • Mabadiliko kwenye seli zako za damu (seli nyekundu za damu, seli nyeupe za damu, na chembe sahani)