Shambulio la moyo ni nini?
Shambulio la moyo ni wakati mtiririko wa damu kwenye sehemu ya moyo wako umezuiwa ghafla na sehemu ya misuli ya moyo wako inakufa.
Nenda kwenye kitengo cha dharura na utafune tembe ya aspirini ikiwa unafikiri kuwa unapata shambulio la moyo
Huenda ukahisi shinikizo kwenye kifua, kushindwa kupumua, na hisia ya uchovu ikiwa unapata tatizo la moyo
Wakati mwingine shambulio la moyo linaweza kusababisha dalili ndogo au lisisababishe dalili zozote (shambulizi tuli la moyo)
Madaktari hufanya vipimo vya damu na ECG/EKG (elektrokadiografia) ikiwa una dalili za shambulio la moyo
Daktari atakupa dawa na kukutibu ili kujaribu kuelekeza damu zaidi kwenye sehemu ya moyo wako iliyoathirika
Je, ni nini husababisha shambulio la moyo?
Moyo ni msuli unaosukuma damu. Kama ilivyo kwa misuli yote, moyo unahitaji damu ya kutosha ili kufanya kazi. Damu inayosukumwa moyoni haifikii msuli wa moyo. Badala yake, msuli wa moyo hulishwa na ateri zake zenyewe. Ateri hizi zinaitwa ateri za moyo.
Mashambulizi mengi ya moyo hutokea wakati mojawapo ya ateri zako za moyo imezuiwa ghafla na damu iliyoganda.
Kwa kawaida, damu huganda kwenye ateri za moyo ukiwa na tatizo la atherosklerosisi:
Usanisi wa mishipa ya damu unajulikana kama kugandamana kwa ateri
Usanisi wa miship ya damu ni pale kolesteroli na utando wa mafuta mengine unarundika polepole kwenye ateri zako
Mrundiko huu unaitwa atheroma au utando
Utando unaweza kupasuka ghafla, na kusababisha donge la damu ambalo linaziba ateri
Ateri iliyozibwa hairuhusu damu ipite hadi kwenye sehemu ya musuli wa moyo wako. Mtiririko wa damu ukikatishwa kwa zaidi ya dakika chache, sehemu hiyo ya musuli wa moyo wako hufa. Musuli uliokufa hauwezi kupiga damu, kwa hivyo moyo wako huwa dhaifu. Midundo ya moyo wako inaweza pia kuathiriwa, na kuufanya upige kwa haraka sana au polepole sana. Wakati mwingine, moyo wako utasimama kabisa (mshtuko wa moyo) na utakufa.
Sehemu ya musuli wa moyo wako inapokufa, huwa hairudi. Musuli uliokufa hubadilika na kuwa tishu ya kovu.
Dalili za shambulio la moyo ni zipi?
Dalili za shambulio la moyo ni sawa na za angina, lakini maumivu huwa makali zaidi, yanadumu kwa muda mrefu, na hayapungui unapopumzika.
Huenda ukahisi maumivu katikati ya kifua
Maumivu yanaweza kusambaa mgongoni, kwenye taya, au mkono wa kushoto
Japo ni nadra, wakati mwinigne maumivu husambaa kwenye mkono wa kulia
Maumivu yanaweza kutokea kwenye sehemu moja au zaidi kati ya hizi na wala si kwenye kifua
Huenda ukahisi woga au kutokwa jasho
Midomo, mikono, au miguu yako huenda ikabadilika na kuwa bluu kidogo
Je, madaktari wanawezaje kujua kama nina shambulio la moyo?
Madaktari hufanya vipimo kama vile:
ECG/EKG—kipimo cha kuchunguza jins moyo wako unavyofanya kazi
Kufanya vipimo vya damu kuchunguza elementi fulani zinazoonyesha matatizo ya moyo
Madaktari hutibu vipi shambulio la moyo?
Utalazwa hospitalini. Madaktari watajaribu:
Kufungua ateri iliyozibwa ili kuokoa kiwango kikubwa cha musuli wa moyo wako kadiri iwezekanavyo
Kutibu tatizo lililosababisha shambulio la moyo wako
Madaktari pia:
Kudhibiti mapigo ya moyo wako na shinikizo la damu
Kukupa dawa za kuzuia damu kuganda
Kukupa dawa za kufanya moyo upige kawaida
Watafungua ateri zilizozibwa
Kwa kutegemea mahali ateri zako za moyo zimezibwa, madkatra wanaweza:
Kukupatia dawa kupitia kwenye mshipa ili kuyeyusha damu iliyoganda
Kufanya upasuaji wa kufungua mshipa
Kufanya upasuaji wa kukwepa
Dawa za kuyeyusha damu iliyoganda unayopewa kupitia kwenye mshipa (IV) zinaweza kufungua ateri ya moyo iliyozibwa. Hata hivyo, dawa hizo hufanya kazi iwapo tu utazipata ndani ya saa chache baada ya shambulio la moyo wako kuanza. Pia, dawa za kuyeyusha damu iliyoganda hazifai kwa kila mtu. Huenda zisiwe salama kwa watu waliopata kiharusi au upasuaji mkubwa hivi majuzi, au watu ambao wana shinikizo la damu la juu.
Wakati wa upasuaji wa kufungua mshipa:
Daktari hutia mrija mwembamba, unaoweza kupinda (katheta) kwenye mshipa wa sehemu ya juu ya mguu wako (kinena) au kwenye kifundo cha mkono
Katheta inasukumwa ndani kwenye ateri hadi kwenye moyo wako kisha kwenye moja ya ateri za moyo
Puto ndogo kwenye ncha ya katheta inatiwa hewa
Puto husukuma na kuzibua mshipa
Kisha daktari anatia mrija wenye wavu (kipanuzi) mwisho wa katheta na kuisogeza sehemu iliyozibwa.
Mrija wenye wavu husaidia kupanua sehemu iliyozibwa
Wakati wa upasuaji wa kupandikiza mshipa:
Daktari huchukua kipande cha ateri au mshipa usio na tatizo kutoka sehemu nyingine ya mwili wako
Anapandikiza ncha moja ya kipande hicho cha ateri au mshipa kwenye aota yako (mshipa mkuu unaobeba damu kutoka kwenye moyo hadi sehemu nyingine zote za mwili)
Anapachika upande wa pili wa ateri yako iliyoziba bila kupitia sehemu hiyo
Kisha damu yako inatiririka kupitia mkondo huu mpya, bila kizuizi
Kutibu kisababishi cha shambulio la moyo wako
Kutibu tatizo lililosababisha shambulio la moyo wako, kwa kawaida madaktari hukupa:
Dawa za kupunguza kolesteroli yako
Dawa za kupunguza shinikizo la damu
Daktari pia atakuruhusu ubadili tabia zozote zinazoumiza moyo wako, kama vile kuvuta sigara, kutofanya mazoezi, na kutokula lishe bora.
Je, ninawezaje kuzuia shambulio la moyo?
Epuka tabia zinazoweza kuudhuru moyo wako
Kula vyakula bora kwa afya, kama vile matunda na mboga na vyakula vingine vyenye nyuzinyuzi kwa wingi
Kula mafuta kidogo kutoka kwenye nyama, maziwa, na vyakula vilivyotengenezwa viwandani (kama vile piza iliyogandishwa au chakula kinachopashwa moto kwa maikrowevu)—zungumza na daktari wako kuhusu kiasi na aina za mafuta unazopaswa kula
Kupunguza uzani ikiwa unahitaji
Kufanya mazoezi kwa kutumia uzani au kutembea
Kuacha kuvuta sigara, kunywa pombe, au kutumia dawa haramu—inaweza kuwa vigumu kuacha kutumia dawa hizi, kwa hivyo zungumza na daktari au mshauri wako wa kisaikolojia kuhusu jinsi ya kupata usaidizi
Kumeza dawa zako inavyofaa
Kumbuka kutumia dawa zozote ulizoagizwa na daktari wako, kama vile dawa za kolesteroli ya juu, shinikizo la juu la damu, au ugonjwa wa kisukari
Ikiwa umewahi kupata shambulio la moyo, mwulize daktari wako kuhusu kutumia kipimo kidogo cha aspirini kila siku ili kusaidia kuzuia shambulio la pili la moyo.