Ugonjwa wa Shida ya Kupumua kwa Watoto Wachanga

Imepitiwa/Imerekebishwa Oct 2022

Ugonjwa wa shida ya kupumua kwa watoto waliozaliwa karibuni ni nini?

Upumuaji unahusiana na kupumua. Ugonjwa wa shida ya kupumua ni aina ya tatizo la kupumua ambalo linaweza kuwapata watoto waliozaliwa hivi karibuni.

  • Ugonjwa wa shida ya kupumua hutokea pale mapafu ya mtoto wako yanapokuwa magumu na hayawezi kubaki wazi yakashikilia pumzi

  • Hutokea pale mapafu ya mtoto wako yanaposhindwa kuunda safaktanti ya kutosha, dutu ambayo husaidia mapafu kubaki wazi

  • Hutokea zaidi kwa watoto waliozaliwa kabla ya wakati wao

  • Ikiwa mtoto wako atazaliwa mapema sana, madaktari watakupatia dawa ambayo itasaidia mapafu ya mtoto wako kuunda safaktanti

  • Baada ya kuzaliwa, madaktari huweka dawa chini ya bomba la pumzi la mtoto wako na kumpatia oksijeni

Je, nini husababisha ugonjwa wa shida ya kupumua?

Kabla ya kuzaliwa, mapafu yako huwa yamefungwa. Mara baada ya kuzaliwa, mtoto wako huvuta pumzi kwa nguvu ili kufungua mapafu na kuyajaza hewa. Ndani ya mapafu kumepakwa dutu ambayo huyafanya yafunguke kwa urahisi. Dutu hiyo huitwa safaktanti.

Watoto waliozaliwa mapema sana (watoto waliozaliwa kabla ya muda wao) huwa hawana safaktanti ya kutosha. Mapafu yao ni magumu kufunguka na mtoto anaweza kupata tatizo la kupumua.

Kwa kawaida ugonjwa wa shida ya kupumua hutokea kwa:

  • Watoto waliowahi kuzaliwa kwa zaidi ya mwezi mmoja

Jinsi mtoto wako anavyozaliwa mapema, ndivyo alivyo na nafasi kubwa ya kupata ugonjwa wa shida ya kupumua. Vigezo vingine vya hatari ni pamoja na:

Zipi ni dalili za ugonjwa wa shida ya kupumua?

Dalili huanza mara baada ya kuzaliwa au ndani ya saa chache. Watoto wachanga wana dalili kama vile:

  • Kupumua haraka

  • Inaonekana anatatizika kupumua

  • Tundu za pua zenye kutanuka wakati wa kuvuta hewa ndani

  • Kukoroma ukitoa pumzi

  • Ngozi ya bluu inayosababishwa na viwango vya chini vya oksijeni

Iwapo hatatibiwa, hali ya upumuaji ya mtoto wako itakuwa mbaya. Ukosefu wa oksijeni unaweza kusababisha uharibifu wa ubongo au matatizo mengine.

Madaktari wanawezaje kujua ikiwa mtoto wangu ana ugonjwa wa shida ya kupumua?

Madaktari hushuku uwepo wa ugonjwa wa shida ya kupumua kulingana na dalili za mtoto wako. Ili kuwa na uhakika:

  • Watachunguza kiwango cha oksijeni cha mtoto wako

  • Watapiga eksirei ya kifua

Je, madaktari wanatibu vipi ugonjwa wa shida ya kupumua?

Madaktari wanatibu ugonjwa wa shida ya kupumua kwa watoto waliozaliwa karibuni kwa:

  • Kumpatia mtoto wako oksijeni ya ziada kupitia mipira ya pua au mfuniko wa plastiki

  • Kutumia mashine kumsaidia mtoto wako kupumua, iwapo mtoto wako anapata shida sana

  • Kumpatia safaktanti ya bandia kupitia bomba liliwekwa chini ya bomba la pumzi

Ikiwa una uwezekano wa kujifungua mtoto njiti, madaktari watakuchoma sindano ya kotikosteroidi. Dawa hii husaidia mapafu ya mtoto wako kuunda safaktanti na husaidia kuzuia ugonjwa wa shida ya kupumua.

Ikiwa mtoto wako atawahi sana kuzaliwa, madaktari wanaweza kumpatia mtoto wako safaktanti hata kabla ya ugonjwa wa shida ya kupumua kuanza.