Ukuaji usio wa Kawaida wa Seli na Tishu za Mapafu (BDP)

Imepitiwa/Imerekebishwa Oct 2022

Ukuaji usio wa kawaida wa seli na tishu za mapafu (BDP) ni nini?

Ukuaji usio wa kawaida wa seli na tishu za mapafu (BDP) ni uharibifu wa mapafu wa muda mrefu unaotendeka kwa watoto wengine waliokuwa na matatizo mabaya sana ya kupumua wakati wa kuzaliwa.

Mara nyingi BDP hutokea kwa watoto ambao waliwekwa kwenye mashine ya kusaidia kupumua au ambao walihitaji kuwekewa oksijeni kwa kipindi kirefu katika siku za mwanzo za maisha yao.

  • Mara nyingi BDP huwapata sana watoto waliozaliwa kabla ya wakati wao

  • Uharibifu wa mapafu unaotokana na BPD huwafanya watoto wahitaji oksijeni ya ziada

  • Watoto wengi hupata ahueni baada ya miezi kadhaa, lakini hali ikiwa mbaya inaweza kuhatarisha maisha

  • BPD inaweza kupunguza kasi ya ukuaji na maendeleo ya mtoto wako na kuongeza hatari ya kupata pumu au nimonia

Je, nini husababisha BPD?

Iwapo mtoto wako ana shida ya kupumua, mashine ya kusaidia kupumua na oksijeni ya ziada inaweza kuokoa maisha yake. Lakini mashine ya kusaidia kupumua na oksijeni inaweza kuharibu mapafu ya mtoto wako ikiwa vitatumika kwa kipindi kirefu.

Kuna uwezekano mkubwa wa kutokea kwa uharibifu wa mapafu iwapo mtoto wako:

  • Amezaliwa kabla ya muda wake

  • Ana tatizo kubwa la mapafu, kama ugonjwa wa shida ya kupumua

  • Alipata maambukizi makali akiwa kwenye tumbo la uzazi au mara baada ya kuzaliwa

Zipi ni dalili za BPD?

Dalili kwa watoto hujumuisha:

  • Kupumua haraka

  • Inaonekana anatatizika kupumua

  • Ngozi ya bluu inayosababishwa na viwango vya chini vya oksijeni

Madaktari wanawezaje kujua ikiwa mtoto wangu ana BPD?

Madaktari hushuku uwepo wa BPD ikiwa mtoto wako:

  • Alizaliwa akiwa njiti na alihitaji mashine ya kumsaidia kupumua kwa kipindi kirefu

  • Anaendelea kuhitaji oksijeni ya ziada au kuwekwa kwenye mashine ya kumsaidia kupumua baada ya kupata ahueni ya tatizo la mapafu la hapo mwanzo

Ili kuwa na uhakika madaktari watafanya:

Je, madaktari hutibu vipi BPD?

Ili kutibu BPD, madaktari:

  • Watampatia oksijeni mtoto wako kupitia bomba lililowekwa kwenye pua zake

  • Watamfanya mtoto wako anywe maziwa ya mama ya ziada au maziwa ya kopo ili kusaidia kukua kwa mapafu ya mtoto wako

  • Watampatia dawa ya kumfanya mtoto wako akojoe ili kupunguza majimaji ya ziada mwilini, ikijumuisha mapafu

Mtoto wako akiondoka hospitalini, madaktari:

  • Watakufanya uweke mtoto wako mbali na moshi wa sigara

  • Watampatia mtoto wako dawa na chanjo ya mafua ili kuzuia maambukizi ya mapafu

Watoto wengi hupata ahueni baada ya miezi kadhaa, lakini mtoto wako anaweza kuwa na uwezekano mkubwa wa kupata pumu au nimonia hapo baadaye maishani.