Tatizo la Kukosa Utulivu

Imepitiwa/Imerekebishwa Sept 2023

Tatizo la kukosa utulivu ni nini?

Tatizo la kukosa utulivu (ADHD) ni tatizo la ubongo ambalo linafanya iwe vigumu kuzingatia na kuweka umakini na kukaa kwa utulivu. Mara nyingi husababisha matatizo hsuleni na nyumbani.

Dalili za ADHD zinaweza kuwa ndogo au kubwa Maeneo fulani (kama vile shule) yanaweza kufanya ziwe mbaya zaidi.

  • ADHD inaanza wakati wa utotoni, mara nyingi kufikia umri wa miaka 4

  • ADHD wakati mwingine inaondoka kadiri mtoto anapokuwa mkubwa, lakini watu wengi wanaendelea kuwa na tatizo hili wakiwa watu wazima

  • Watoto wenye ADHD wana tatizo la kutoweza kumakinika na wana shughuli nyingi (amilifu kupita kiasi)

  • Watoto wengi wenye ADHD pia wana matatizo ya kujifunza

  • Dawa mara nyingi zinawasaidia watoto wenye ADHD

Je, ADHD husababishwa na nini?

Madaktari hawana uhakika kwa nini mtoto anapata ADHD. Pengine husababishwa na matatizo ya jinsi ubongo ulivyoundwa wakati mtoto anakua tumboni kabla ya kuzaliwa. Mara chache sana, matatizo baada ya kuzaliwa yanasababisha ADHD.

ADHD ni tatizo la ubongo na wala si tatizo la tabia.

Watoto wana uwezekano mkobwa wa kupata ADHD ikiwa:

  • Wana ndugu mwenye ADHD (unarithishwa kwenye familia)

  • Alikuwa ana uzito chini ya 3 wakati wa kuzaliwa

  • Alipata jeraha kichwani au maambukizi ya ubongo

  • Alikuwa katika mazingira ya madini ya risasi, pombe, umbaku au kokeni kabla ya kuzaliwa

Dalili za ADHD ni zipi?

ADHD kwa watoto

Dalili za ADHD kwa watoto:

  • Kutoweza kumakinika

  • Shughuli za kimwili nyingi kupita kiasi

  • Mwenye mihemko sana (anafanya vitu bila kufikiri)

Ukilinganisha na watu wazima, watoto wote wana shida kidogo ya kuwa na umakinifu na kukaa wakiwa wametulia. Hata hivyo, watoto wenye ADHD wana matatizo zaidi kuliko watoto wengine

Ishara za matatizo ya kwua na umakini:

  • Kutosikiliza anaposemeshwa

  • Kutofuata maelekezo au kumaliza kazi

  • Kuepuka kazi ambazo zinahitaji kufikiri sana

  • Kupata shida kupangilia kazi

  • Kuchanganywa kwa urahisi

  • Kupoteza au kusahau vitu

Ishara za kukosa utulivu:

  • Kuriaria kwa mikono au miguu au kutembeza miguu

  • Kutoka kwenye viti vyao wakiwa shuleni au nyumbani

  • Kukimbia au kupanda juu ya vitu kuliko kawaida

  • Kupata shida kucheza kwa utulivu

  • Kuzungumza zaidi kuliko kawaida

Ishara za kufanya mambo kwa mihemko:

  • Kutoa majibu kabla swali halijakamilika kuulizwa

  • Kupata shida kusubiri zamu yake

  • Kuzungumza wakati si zamu yake kuwakatiza wengine

Watoto wengi wenye ADHD wanapunguza kidogo hali ya kutokuwa na utulivu wanapokuwa wakubwa na wanaweza kukabiliana vizuri na mazingira. Wengi watakuwa na kuwa watu wazima wenye tija na wabunifu. Hata hivyo, ADHD isiyotibika inaweza kusababisha uwezekano wa matumizi mabaya ya pombe, dawa za kulevya au kujinyonga.

ADHD kwa watu wazima

Dalili za ADHD kwa watu wazima:

  • Kupata shida kumakinika

  • Kupata shida kukamilisha kazi

  • Kutokuwa na utulivu

  • Mihemko ya hisia

  • Kutokuwa mvumilivu

  • Kupata shida kwenye mahusiano

Madaktari wanawezaje kujua ikiwa mtoto wangu ana ADHD?

Madaktari hushuku uwepo wa ADHD kutokana na dalili za mtoto wako. Hakuna vipimo vyovyote ambavyo vinaweza kusema kwa uhakika kuwa mtoto wako ana ADHD au la. Hata hivyo, madaktari wanaweza kuangalia endapo dalili za mtoto wako zinasababishwa na tatizo jingine, kama vile:

Je, madaktari wanatibu vipi ADHD?

Kumfokea au kumwadhibu mtoto wako hakusaidii. Madaktari watamtibu mtoto wako kwa kutumia:

  • Ushauri nasaha kuhusu namna ya kuboresha tabia (tiba ya tabia)

  • Dawa

Madaktari na washauri nasaha wanaweza kupendekeza kukusaidia wewe na mtoto wako kushughulika na ADHD. Mambo ambayo mara nyingi husaidia hujumuisha:

  • Kuweka utaratibu nyumbani na shuleni

  • Kutoa zawadi ndogo kwa tabia nzuri

  • Kudumu kuwa thabiti kuhusu tabia unayoitarajia

  • Kufanya kazi na walimu ili kutoa kazi na masomo mafupi shuleni

Mtoto mwenye ADHD huenda akahitaji usaidizi maalumu shuleni. Nchini Marekani, Sheria ya Elimu ya Watu Wenye Ulemavu (IDEA) inazitaka shule za umma kutoa elimu ya nzuri na ya bila malipo kwa watoto wenye ADHD.

Dawa za kutibu ADHD ni dawa kama vile Ritalin® na nyinginezo ambazo kimsingi zinaamsha ubongo. Unaweza kudhani mtoto wako tayari amechochewa sana. Hata hivyo, dawa hizi zinaamsha sehemu za ubongo wako ambazo zinasaidia mtoto wako kuwa na umakini.

Dawa za kuamsha ubongo zinaweza kuwa na athari:

  • Kushindwa kulala

  • Kupoteza hamu ya kula (watoto wanaweza kula kidogo sana na wakashindwa kukua vizuri)

  • Mapigo ya mayo ya haraka na shinikizo la juu la damu

Ili kupunguza athari, daktari wako anaweza kupendekeza uache kutumia dawa siku za wikendi na wakati wa likizo.