Ugonjwa wa kidole tumbo kwa Watoto

Imepitiwa/Imerekebishwa Oct 2023

Je, ugonjwa wa kidole tumbo ni nini?

Ugonjwa wa kidole tumbo ni hali ya kuvimba (kutuna) na maambukizi kwenye kidole tumbo chako. Kidole tumbo ni kiungo kidogo chenye umbo la kidole kilichounganishwa na utumbo wako mpana.

Apendiksi ni kiungo ambacho hakina kazi mahususi. auhitaji kuwa na apendiksi yako ili kuishi maisha yenye afya.

  • Ugonjwa wa kidole tumbo mara nyingi hutokea kwa vijana na watu wazima wachanga na haitokei mara nyingi kabla ya umri wa mwaka 1

  • Dalili zinajumuisha maumivu ya tumbo (kwa kawaida katika sehemu ya chini ya tumbo upande wa kulia), homa ya chini (100° hadi 101° F au sentigredi [37.7° hadi 38.3°])

  • Inaweza kuwa ngumu kwa madaktari kubaini ikiwa mtoto wako ana ugonjwa wa kidole tumbo au tatizo lingine—watafanya vipimo vya damu na picha ya kutumia mawimbi ya sauti

  • Ugonjwa wa kidole tumbo ni dharura ya kimatibabu na mtoto wako atahitaji kufanyiwa upasuaji

Je, ugonjwa wa kidole tumbo husababishwa na nini?

Ugonjwa wa kidole tumbo wakati mwingine hutokea wakati kidole tumbo kimezibwa na:

  • Kinyesi kigumu (mavi)

  • Nodi za limfu (viungo vidogo vyenye umbo la haragwe vinavyosaidia kupigana na maambukizi) kwenye utumbo vinavyovimba kwa sababu ya maambukizi

Bila kujali kile kinachoziba, apendiksi huvimba na bakteria kukua. Ikiwa ii haitatibiwa, apendiksi inaweza kufunguka na kusababisha maambukizi ndani ya tumbo lako (inaitwa peritonitisi), ambayo inaweza kuwa hatari.

Je, dalili za ugonjwa wa kidole tumbo ni zipi?

Dalili zinajumuisha:

  • Maumivu katika sehemu ya katikati ya tumbo yanayosonga hadi sehemu ya chini ya upande wa kulia

  • Kwa watoto, maumivu haya yanaweza kutokea katika sehemu yote ya tumbo

  • Kutapika na kukosa hamu ya kula

  • Homa ya chini ya Farenheiti ya nyuzi 100 hadi nyuzi 101 (sentigredi za nyuzi 37.7 hadi nyuzi 38.3)

Madaktari wanawezaje kujua kama mtoto wangu ana ugonjwa wa kidole tumbo?

Inaweza kuwa vigumu kuwa na uhakika kuwa mtoto wako ana ugonjwa wa kidole tumbo. Madaktari wakifikiria kuwa mtoto wako ana ugonjwa wa kidole tumbo, watafanya:

  • Vipimo vya damu

  • Kipimo cha picha kwa kutumia mawimbi ya sauti

Ikiwa matokeo ya kipimo cha picha kwa kutumia mawimbi ya sauti hayako wazi, madaktari wanaweza:

Je, ugonjwa wa kidole tumbo hutibiwa vipi?

Madaktari hutibu ugonjwa wa kidole tumbo kwa kufanya upasuaji ili kuondoa kidole tumbo (upasuaji wa kuondoa kidole tumbo). Ugonjwa wa kidole tumbo usiotibiwa unaweza kuwa na madhara hatari.

Wakati mzuri zaidi wa kufanya upasuaji ni kabla ya kidole tumbo kupasuka. Ikiwa tayari kidole tumbo kimepasuka, daktari:

  • Hutoa kidole tumbo

  • Huosha vitu vilivyo ndani ya tumbo ya mtoto wako kwa kutumia kiowevu

  • Hutoa dawa za kuua bakteria kwa siku kadhaa

  • Hukagua matatizo, kama vile maambukizi au kuziba kwa utumbo