Uvimbe wa Meckel

Imepitiwa/Imerekebishwa Oct 2023

Je, divatikulamu ya Meckel ni nini?

Divatikulamu ya Meckel (inayojulikana pia kama divatikulamu yake Mackel) ni kifuko kidogo kwenye utando wa utumbo mdogo. `Baadhi ya watoto wachanga wako nayo wakizaliwa. Kwa kawaida divatikulamu haisababishi dalili, kwa hivyo watu wengi hawajui kama wanayo.

Uvimbe wa Meckel

  • Baadhi ya watoto wachanga au watoto walio na divatikulamu ya Meckel wanaweza kuwa na hali ya kuvuja damu isiyo na maumivu ambayo hutokea kwenye kinyesi chao (haja kubwa)

  • Wakati mwingine, divatikulamu inaweza kuambukizwa

  • Madaktari watafanya upasuaji ili kuondoa divatikulamu ambayo inavuja damu zaidi au kusababisha dalili zingine

Dalili za Divatikulamu ya Meckel ni zipi?

Divatikulamu ya Meckel haisababishi dalili kwa watu wengi waliyo nayo. Hata hivyo, wakati mwingine mtoto ana dalili kama vile: 

  • Kinyesi chenye rangi nyekundu ang'avu, kutu, rangi ya zambarau au cheusi kwa sababu ya divatikulamu inayovuja damu—hii huwapata zaidi watoto wenye umri chini ya miaka 5

  • Wakati mwingine, maumivu makali ya tumbo, ulaini wa tumbo na kutapika ikiwa divatikulamu inaambukizwa au kuwasha—hii inaitwa divatikulaitisi

Madaktari wanawezaje kujua kama mtoto wangu ana divatikulamu ya Meckel? 

Madaktari wakishuku kuwa mtoto wako ana divatikulamu ya Meckel, wanaweza kufanya vipimo kama vile:

  • Uchanganuaji wa Mackel, ambapo madaktari watapea mtoto wako kidogo cha dutu ya mionzi isiyo na madhara kupitia kwenye mshipa na kuchukua picha za utumbo mdogo kwa kutumia kamera maalum

  • Endoskopia ya kapsuli ya video, ambapo mtoto wako anameza kamera ndogo zaidi ambayo inapiga picha inapopita kwenye njia ya mmeng'enyo wa chakula, ikijumuisha utumbo

  • Endoskopia, ambapo madaktari huweka bomba ndogo nyepesi ya kutazama kwenye tundu lako la haja kubwa (shimo lililo kwenye matako ambapo kinyesi hutokea) ili kuona utumbo mdogo

Madaktari wanatibuje divatikulamu ya Meckel?

Madaktari hawatatibu divatikulamu isipokuwa kama inasababisha dalili.

Ikiwa mtoto wako ana dalili kama vile maumivu au kuvuja damu sana:

  • Madaktari watafanya upasuaji ili kuondoa divatikulamu