Ostiyomayelaitisi

(Maambukizi ya mfupa)

Imepitiwa/Imerekebishwa Feb 2023

Ostiyomayelaitisi ni nini?

Ostiyomayelaitisi ni maambukizi ya mfupa.

  • Mfupa ni tishu hai na unaweza kuambukizwa kama sehemu nyingine yoyote ya mwili wako

  • Maambukizi huingia kwenye mfupa kupitia damu yako au kutoka kwenye tishu ya karibu yenye maambukizi au kidonda kilicho wazi

  • Unaweza kuwa na maumivu katika mfupa wako, homa, na kupoteza uzani

  • Uchanganuzi wa CT (tomografia ya kompyuta), au MRI (upigaji picha kwa mvumo wa sumaku)

  • Utahitaji kutumia dawa za kuua bakteria kwa wiki kadhaa au uwezekano wa kufanyiwa upasuaji kwa ajili ya kutibu ostiyomayelaitisi

Maambukizi yakiwa mabaya, baadhi ya sehemu za mfupa zinaweza kufa, hivyo kufanya maambukizi kuwa magumu kutibu.

Wakati mwingine maambukizi huenea kutoka kwa mfupa wako hadi kwenye ngozi na misuli iliyo karibu.

Je, nini husababisha ostiyomayelaitisi?

Kwa kawaida maambukizi ya mifupa husababishwa na bakteria wanao:

  • Enea kutoka kwa ngozi iliyo karibu iliyoambukizwa

  • Ingia kupitia kidonda kilichochimba juu ya mfupa

Ni mara chache bakteria:

  • Husafiri kupitia mtiririko wa damu kutokana na maambukizi katika sehemu nyingine ya mwili wako

  • Huingia wakati mfupa uliovunjika umetoboa ngozi

  • Ni matatizo ya upasuaji wa mfupa au kiungo

Una uwezekano mkubwa wa kupata maambukizi ya mifupa ostiyomayelaitisi kama:

Zipi ni dalili za ostiyomayelaitisi?

Dalili za maambukizi ya mifupa ostiyomayelaitisi ni pamoja na:

  • Homa

  • Maumivu kwenye mifupa iliyoambukizwa

  • Sehemu nyekundu, ya vuguvugu, iliyovimba juu ya mfupa wenye maambukizi

  • Kupungua uzani na uchovu

Madaktari wanawezaje kujua ikiwa nina maambukizi ya mifupa ostiyomayelaitisi?

Madaktari hufanya:

Ikiwa vipimo hivi vinaonyesha uwepo wa ostiyomayelaitisi, basi madaktari wanaweza:

  • Kuchukua sampuli ya sehemu iliyoambukizwa kwa kutumia sindano au kwa upasuaji

Je, madaktari wanatibu vipi maambukizi ya mifupa ostiyomayelaitisi?

Madaktari hutibu maambukizi ya mifupa ostiyomayelaitisi kwa kutumia:

  • Dawa za kuua bakteria zinazoingizwa kwa njia ya mshipa

Unaweza kutakiwa kutumia dawa za kuua bakteria kwa wiki 4 hadi 8, hasa ikiwa umekuwa na maambukizi kwa muda mrefu.

Ikiwa wewe ni mgonjwa au kuna mifupa mingi iliyokufa, madaktari wanaweza:

  • Kufanya upasuaji ili kuondoa mfupa ulioambukizwa na kufa