Je, lukemia ni nini?
Lukemia ni saratani ya seli nyeupe za damu. Seli nyeupe za damu zina kazi nyingi, ikiwemo kusaidia mfumo wa kingamaradhi ya mwili wako kukabiliana na maambukizi. Seli nyeupe za damu hutengenezwa kwenye uboho wako, tishu nyororo ndani ya mifupa yako.
Ukiwa na lukemia, idadi yako ya seli nyeupe za damu iko juu sana. Hata hivyo, seli nyeupe za damu zenye saratani hazifanyi kazi ipasavyo, hivyo kuna uwezekano wa kupata maambukizi. Maambukizi hayo yanaweza kuhatarisha maisha.
Pia, seli nyeupe za damu zenye saratani hujaa kwenye uboho wako hivyo huwezi kutengeneza seli za damu za kawaida kama vile:
Seli nyekundu za damu (husababisha anemia)
Seli nyeupe za damu za kawaida (huongeza hatari ya maambukizi)
Chembe sahani (huongeza hatari ya kuvuja damu)
Kuna aina nyingi tofauti za seli nyeupe za damu lakini aina 2 kuu tu za lukemia:
Lukemia ya limfu: saratani inayoathiri limfu, ambayo ni aina moja ya seli nyeupe za damu
Lukemia ya uboho: saratani inayoathiri aina nyingine zote za seli nyeupe za damu
Lukemia ya limfu na uboho inaweza kuwa kali au sugu:
Kali: saratani ya seli changa ambayo huenea haraka na inaweza kusababisha kifo ndani ya miezi 3 hadi 6 isipotibiwa
Sugu: saratani ya seli zilizokomaa inayoenea polepole
Lukemia ya Limfosaiti ya Muda Mrefu (CLL) ni nini?
Lukemia ya limfosaiti ya muda mrefu (CLL) ni aina ya saratani ya seli nyeupe za damu ambayo inaathiri lymphocyte, ambayo kwa kawaida husaidia mwili wako kupigana na maambukizi. Katika CLL, lymphocyte zako kugeuka kuwa seli za saratani. Seli hizi za saratani huchukua nafasi ya lymphocyte zenye afya kwenye damu yako, uboho na vinundu vya limfu (viungo vya ukubwa wa dengu mwili wako mzima ambavyo hupigana na maambukizi).
Ugonjwa wa CLL kwa kawaida hutokea kwa watu wazima wenye umri zaidi ya miaka 60 na kuna uwezekano mkubwa wa kuathiri wanaume kuliko wanawake
CLL ni nadra sana kwa watoto
Unaweza kosa kuwa na dalili au unaweza kuwa na dalili za kawaida kama vile uchovu, kukosa hamu, kupungua uzani na vinundu vya limfu vilivyovimba
Ili kujua kama una CLL, madaktari hufanya vipimo vya damu na kupima uboho wako
Lukemia ya limfosaiti ya muda mrefu hukua polepole zaidi na huenda isihitaji matibabu kwa miaka mingi
Watu walio na CLL mara nyingi huishi miaka 10 hadi 20 au zaidi baada ya madaktari kutambua uwepo wa ugonjwa
Aina za CLL zinajumuisha:
Lukemia ya seli-B—hii ndiyo inatokea sana
Lukemia ya seli zenye nywele
Lukemia ya seli-T
Je, dalili za CLL ni zipi?
Watu wengi hawana dalili kwanza.
Dalili za baadaye zinaweza kujumuisha:
Vinundu vya limfu vilivyovimba (ogani zenye ukubwa unaolingana na dengu kwenye mwili mzima ambazo zinasaidia kupigana na maambukizi)
Kuhisi udhaifu na uchovu
Kutokuwa na njaa na kupoteza uzani
Kukosa pumzi unapofanya mazoezi
Kuhisi kujaa kwenye eneo la tumbo yako (kutokana na ini na wengu uliovimba)
Ngozi kuonekana hafifu
Kuvimba kwa urahisi
Una uwezekano mkubwa wa kupata saratani zingine, kama vile saratani za mgozi au mapafu.
Madaktari wanawezaje kujua kama nina CLL?
Ili kujua kama una CLL, madaktari watafanya haya:
Fanya vipimo vya damu
Chukua sampuli ya uboho wako ili upimwe (kipimo cha uboho)
Wakati mwingine madaktari hupata kuwa una CLL wakati wanafanya vipimo vya damu ili kuangalia matatizo mengine ya afya.
Madaktari hutibu vipi CLL?
Unaweza kosa kuhitaji matibabu yoyote kwa miaka.
Wakati unahitaji matibabu, yanaweza kujumuisha:
Kotikosteroidi
Kingamwili za monokrono (dawa ambazo husaidia mfumo wako wa kingamwili kupigana na saratani yako)
Madaktari wanaweza pia kukupatia matibabu kwa ajili ya dalili zingine, ikijumuisha:
kuongezewa damu
Dawa ili kukusaidia kuunda seli nyekundu za damu zaidi
Kuongezewa chembe sahani, ikiwa chembe sahani zako ni kidogo (chembe sahani ni seli za damu ambazo husaidia damu yako kuganda)
Dawa za kuua bakteria kwa ajli ya maambukizi
Tiba ya mionzi kwa ajili ya kuhisi vibaya kutokana na ini au wengu uliovimba