Ugonjwa wa ngozi unaosababishwa na kupitia kugusana

Imepitiwa/Imerekebishwa May 2023

Ugonjwa wa ngozi unaosababishwa na kupitia kugusana ni nini?

Ugonjwa wa ngozi ni istilahi ya jumla inayorejelea mwasho na uvimbaji wa kawaida wa ngozi.

Ugonjwa wa ngozi unaosababishwa na kupitia kugusana ni upele unaosababishwa na kugusa kitu ambacho kinasababisha mjibizo kwenye ngozi yako. Kitu hicho kinaweza kuwasha ngozi yako (ugonjwa wa mwasho wa ngozi unaosababishwa na kugusana au unaosababisha mmenyuko wa mzio) au kusababisha mmenyuko (ugonjwa wa ngozi unaosababishwa na mzio wa kugusana).

  • Maelfu ya vitu vinaweza kusababisha ugonjwa wa ngozi unaosababishwa na kupitia kugusana unaowasha au ugonjwa wa ngozi unaosababishwa na kupitia kugusana wa mzio.

  • Ugonjwa wa ngozi unaosababishwa na kupitia kugusana unaweza kuanza wakati wowote kwenye maisha yako

  • Ikiwa utapata ugonjwa wa ngozi unaosababishwa na kupitia kugusana kutoa kwenye kitu fulani mara moja pengine utaupata kila wakati utakapogusa kitu hicho

  • Njia bora ya kutibu ugonjwa wa ngozi unaosababishwa na kupitia kugusana ni kuepuka kitu chochote kinachousababisha

  • Ugonjwa wa ngozi unaosababishwa na kupitia kugusana unaweza kuchukua wiki 3 kuondoka

  • Kugusa upele hakutaueneza kwa mtu mwingine

Nini kinachosababisha ugonjwa wa ngozi unaosababishwa na kupitia kugusana?

Ugonjwa wa ngozi unaosababishwa na kupitia kugusana unaowasha unasababishwa na vitu vinavyowasha ngozi yako unapovigusa, kama vile:

  • Kemikali, kama vile vifaa vya usafi vya kukaisha maji na vifaa vya kuondoa rangi ya kucha

  • Baadhi ya vipodozi, deodranti na sabuni

  • Pombe ya kusugulia

  • Viyeyushaji thabiti na blichi

  • Mimea fulani, kama vile poinsettias na pilipili

  • Wakati mwingine majimaji ya mwili, kama vile mkojo na mate

Watu wengine wanadhurika kwa urahisi sana na vitu vinavyowasha kuliko wengine.

Ugonjwa wa mzio wa ngozi unaosababishwa na kugusana ni wakati ambapo mfumo wako wa kingamwili unapata mmenyuko kutokana na kitu kilichogusa ngozi yako. Unaweza kuwa na mzio kutokana na vitu vingi mbalimbali, lakini sababu kubwa zaidi ya ugonjwa wa ngozi unaosababishwa na kupitia kugusana wa mzio ni:

  • Mimea fulani, kama vile sumu mwefeu

  • Mpira, ikiwa ni pamoja na latex

  • Dawa za kuua bakteria na dawa nyinginezo zinawekwa kwenye ngozi

  • Manukato na marashi

  • Vihifadhi chakula

  • Baadhi ya metali kama vile nikeli na kobalti

Wakati mwingine unapata ugonjwa wa ngozi unaosababishwa na kupitia kugusana mwanga wa jua unapowaka kwenye ngozi ambayo ina vitu fulani juu yake, kama vile:

  • Vizuia jua

  • Losheni ya kupaka baada ya kunyoa

  • Marashi fulani

  • Dawa fulani za kuua bakteria unazoweka kwenye ngozi yako

  • Lami ya makaa ya mawe

  • Mafuta

  • Mimea

  • Vinyunyizi fulani kama vile viua wadudu

Dalili za ugonjwa wa ngozi unaosababishwa na kupitia kugusana ni zipi?

Dalili zinajumuisha:

  • Kuwashwa na wakati mwingine kuungua au maumivu

  • Vipele vyakundu, wakati mwingine ukiwa na uvimbe au malengelenge madogo

  • Ngozi kavu, yenye magamba au iliyopasuka ikiwa ulipata ugonjwa wa ngozi unaosababishwa na kupitia kugusana muda mrefu uliopita

  • Wekundu zaidi, kutoka machozi na kuvimba ikiwa ngozi itaambukizwa

Madaktari wanawezaje kujua ikiwa nina ugonjwa wa ngozi unaosababishwa na kupitia kugusana?

Kwa kawaida madaktari wanaweza kufahamu kuwa una ugonjwa wa ngozi unaotokana na kugusana kwa kuangalia vipele vyako. Hata hivyo, inaweza kuwa vigumu kujua ni kitu gani hasa kilichosababisha mjibizo.

Ikiwa hujui sababu ya vipele vyako, daktari wako anaweza kufanya vipimo ili kujua nini kilichosababisha. Hizi zinaweza kujumuisha vipimo vya mzio. Katika vipimo vya mzio, daktari wako anaweka viwango vidogo vya vitu tofuati kwenye ngozi yako kuona ikiwa vinaweza kusababisha ugonjwa wa ngozi unaosababishwa na kugusana.

Madaktari wanatibu vipi ugonjwa wa ngozi unaosababishwa na kugusana?

Kwanza madaktari wanatibu ugonjwa wa ngozi unaosababishwa na kugusana kwa kuhakikisha hukutani zaidi na kitu ambacho kimesababisha upele. Mara kitu hicho kinapoondoka, upele hupotea wenyewe.

Mwasho na malengelenge yanaweza kupata unafuu kupitia:

  • Krimu ya kotikosteroidi

  • Vidonge vya antihistamini

  • Kuweka kitambaa kilicholowekwa kwenye maji baridi au aluminum acetate (mchanganyiko wa Burow) kwenye upele mara kadhaa kwa siku

  • Oga kwa maji baridi kwa kuongeza shayiri ya unga laini (bidhaa inayotengenezwa kwa unga laini wa shayiri)

  • Dawa ya kuua bakteria, ikiwa ngozi itaambukizwa

  • Kotikosteroidi ya kunywa na dawa ambazo zinapunguza kasi ya mfumo wa kingamaradhi ikiwa ugonjwa wa ngozi unaosababishwa na kugusana ni mkali

Vidonge vya antihistamini vinaweza kukufanya usinzie, haswa kwa wenye umri zaidi. Kuwa mwangalifu kuhusu kuzitumia ikiwa unahitaji kuendesha gari au kutumia zana za kielekroniki. Kwa upande mwingine, antihistamini inaweza kukusaidia kulala usiku.

Kuna krimu kadhaa za mwasho ambazo unaweza kununua bila kuandikiwa na daktari. Krimu za antihistamini na krimu za kufisha ngozi ganzi zilizo na benzokaini wakati mwingine husababisha madhara kwenye ngozi, hivyo madaktari hawapendelei uzitumie.

Ninawezaje kuzuia ugonjwa wa ngozi unaosababishwa na kugusana?

Epuka kugusana na vitu vinavyowasha ngozi yako au vinavyokusababishia mmenyuko wa mzio.

Ikiwa utagusana na kitu, osha ngozi yako kwa sabuni na maji baada tu ya kugusana. Ikiwa utalazimika kugusa kitu hicho, vaa glavu, nguo au krimu ya kizuizi inayozuia ngozi yako isiguswe.