Nyenzo za Mada

Je, rinaitisi ni nini?

Rinaitisi ni mwako na uvimbe ndani ya pua yako.

  • Kwa kawaida rinaitisi husababishwa na mafua au mizio ya vipindi

  • Utapata pua zinazotoa makamasi, chafya, na vitu kujazana puani

  • Kwa kawaida rinaitisi hupotea yenyewe, lakini madaktari wanaweza kukufanya utumie antihistamini

  • Iwapo mizio hukufanya upate rinaitisi mara kwa mara, unaweza kutakiwa kuchoma sindano za kuzuia mzio

Je, nini husababisha rinaitisi?

Rinaitisi inaweza kusababishwa na:

  • Mmenyuko wa mzio wa kitu fulani, kama vile vumbi, ukungu, chavua, majani, miti, na wanyama (mzio wa rinaitisi)

  • Maambukizi, kama vile mafua ya kawaida

  • Kupumua hewa kavu sana au chafu

Wazee wakati mwingine hupata hali ya kupungua na kukakamaa kwa utando wa tishu za pua zao, hali ambayo husababisha rinaitisi

Je, dalili za rinaitisi ni zipi?

Dalili zinajumuisha:

  • Pua zinazotoa kamasi

  • Pua kufungana

  • Kupiga chafya

Unaweza kuwa na dalili nyingine pia, kutegemea na chanzo cha rinaitisi. Ikiwa ilisababishwa na mizio, unaweza kuwa na mwasho, au macho yenye machozi. Ikiwa rinaitisi yako imetokana na mafua, unaweza kuwa na koo lenye vidonda na kikoho.zi

Je, madaktari wanawezaje kujua kama nina rinaitisi?

Madaktari wanaweza kujua ikiwa una rinaitisi kwa kutegemea na dalili zako.

Je, madaktari hutibu vipi rinaitisi?

Matibabu hutegemea na chanzo cha rinaitisi.

Ikiwa mzio ndio unaosababisha upate rinaitisi, madaktari watakufanya ujiepushe na vitu ambavyo vinakufanya uwe na mzio. Watakutibu kwa:

  • Kotikosteroidi ya kupuliza puani

  • Vidonge vya antihistamini

  • Wakati mwingine, sindano za kuzuia mizio

Madaktari wanaweza kutibu aina zingine za rinaitisi kwa:

  • Dawa za kupaka puani

  • Dawa za kufungua pua (vinyunyizio au vidonge)

  • Kupitisha maji kwenye pua zako (umwagiliaji wa pua)

  • Kilainisha hewa au kiongezaji cha mvuke kwenye hewa ili kuifanya hewa katika nyumba yako iwe na unyevunyevu zaidi