Je, rinaitisi ni nini?
Rinaitisi ni mwako na uvimbe ndani ya pua yako.
Kwa kawaida rinaitisi husababishwa na mafua au mizio ya vipindi
Utapata pua zinazotoa makamasi, chafya, na vitu kujazana puani
Kwa kawaida rinaitisi hupotea yenyewe, lakini madaktari wanaweza kukufanya utumie antihistamini
Iwapo mizio hukufanya upate rinaitisi mara kwa mara, unaweza kutakiwa kuchoma sindano za kuzuia mzio
Je, nini husababisha rinaitisi?
Rinaitisi inaweza kusababishwa na:
Mmenyuko wa mzio wa kitu fulani, kama vile vumbi, ukungu, chavua, majani, miti, na wanyama (mzio wa rinaitisi)
Maambukizi, kama vile mafua ya kawaida
Kupumua hewa kavu sana au chafu
Wazee wakati mwingine hupata hali ya kupungua na kukakamaa kwa utando wa tishu za pua zao, hali ambayo husababisha rinaitisi
Je, dalili za rinaitisi ni zipi?
Dalili zinajumuisha:
Pua zinazotoa kamasi
Pua kufungana
Kupiga chafya
Unaweza kuwa na dalili nyingine pia, kutegemea na chanzo cha rinaitisi. Ikiwa ilisababishwa na mizio, unaweza kuwa na mwasho, au macho yenye machozi. Ikiwa rinaitisi yako imetokana na mafua, unaweza kuwa na koo lenye vidonda na kikoho.zi
Je, madaktari wanawezaje kujua kama nina rinaitisi?
Madaktari wanaweza kujua ikiwa una rinaitisi kwa kutegemea na dalili zako.
Je, madaktari hutibu vipi rinaitisi?
Matibabu hutegemea na chanzo cha rinaitisi.
Ikiwa mzio ndio unaosababisha upate rinaitisi, madaktari watakufanya ujiepushe na vitu ambavyo vinakufanya uwe na mzio. Watakutibu kwa:
Kotikosteroidi ya kupuliza puani
Vidonge vya antihistamini
Wakati mwingine, sindano za kuzuia mizio
Madaktari wanaweza kutibu aina zingine za rinaitisi kwa:
Dawa za kupaka puani
Dawa za kufungua pua (vinyunyizio au vidonge)
Kupitisha maji kwenye pua zako (umwagiliaji wa pua)
Kilainisha hewa au kiongezaji cha mvuke kwenye hewa ili kuifanya hewa katika nyumba yako iwe na unyevunyevu zaidi