Feyokromosaytoma

Imepitiwa/Imerekebishwa Jul 2024

Kuvimba kwa feyokromosaytoma ni nini?

Feyokromosaytoma ni aina ya uvimbe ambayo hutengeneza homoni zinazoongeza shinikizo la damu yako. Feyokromosaytoma nyingi hukua katika tezi za adrenal. Tezi zako za adrenali ziko juu ya figo zako.

  • Baadhi ya feyokromosaitoma zina saratani lakini nyingi hazina

  • Feyokromosaytoma mara nyingi husababishwa na magonjwa ya kijeni

  • Feyokromosaytoma kawaida hutokea kati ya miaka 20 na 40

  • Una shinikizo la juu la damu ambalo wakati mwingine huja na kuondoka

  • Unaweza kuwa na maumivu ya kichwa, kutokwa na jasho, na kuhisi moyo wako ukipiga kwa kasi na kudunda

  • Madaktari kawaida hufanya upasuaji kuondoa feyokromosaytoma

Je, nini husababisha feyokromosaytoma?

Feyokromosaytoma mara nyingi husababishwa na magonjwa adimu ya kijeni kama vile:

Unaweza pia kupata feyokromosaytoma bila kuwa na moja ya magonjwa haya. Madaktari hawajui sababu ya feyokromosaytoma kwa watu hawa.

Zipi ni dalili za feyokromosaytoma?

Dalili zinajumuisha:

  • Moyo unaopiga haraka, unaodunda

  • Kutokwa jasho

  • Kuhisi wepese wa kichwa wakati umesimama

  • Kupumua haraka

  • Ngozi baridi na iliyo na unyevu

  • Maumivu makali ya kichwa

Dalili mara nyingi huja na kuondoka na zinaweza kuwa kama za shambulio la hofu.

Madaktari wanawezaje kujua ikiwa nina feyokromosaytoma?

Madaktari hupima feyokromosaytoma kwa kutumia:

Ikiwa una feyokromosaytoma, madaktari wanaweza pia kufanya vipimo vya jenetiki ili kuona ikiwa hali isiyo ya kawaida husababisha feyokromosaytoma.

Je, madaktari wanatibu vipi feyokromosaytoma?

Madaktari wanakupa dawa ya kudhibiti shinikizo la damu yako na kisha kufanya:

  • Upasuaji wa kuondoa uvimbe