Angiofibroma ya vijana

Imepitiwa/Imerekebishwa Jun 2024

Angiofibroma ya vijana ni nini?

Angiofibroma ya vijana ni mabonge ya nadra ya mishipa ya damu ambayo yanakua mahali ambapo koo na mwanzi wa pua wa mtoto wako zinapatana (karibu na adenoidi).

  • Angiofibroma ya vijana ni za kawaida kwa vijana wa kiume

  • Zinakua polepole na zinaweza kuenea kwenye sehemu kando ya ubongo na tundu la kishimo cha macho

Dalili za angiofibroma ya vijana ni zipi?

  • Pua iliyojaa

  • Maumivu ya kichwa

  • Kutokwa na damu puani ambao kunaweza kuwa kubaya zaidi

  • Uso uliovimba

  • Jicho lililofura

  • Badiliko kwenye umbo la mapua

Madaktari wanawezaje kujua kama mtoto wangu ana angiofibroma ya vijana?

Madakatri kwa kawaida watafanya uchanganuzi wa CT (tomografia ya kompyuta) au MRI (upigaji picha kwa mvumo wa sumaku)

Madaktari hutibu aje angiofibroma ya vijana?

  • Kwa kawaida, madaktari watafanya upasuaji ili kuondoa bonge

  • Madaktari wanaweza pia kutumia tiba ya mionzi, haswa ikiwa bonge ni ngumu kuondolewa kikamilifu au ikirudi