Hipothemia

Imepitiwa/Imerekebishwa Oct 2024

Hipothemia ni nini?

Hipothemia ni hali hatarishi ya joto la chini la mwili, kwa kawaida chini ya 95° F (35° C).

  • Unaweza kupata hipothemia unapokaa katika eneo lenye baridi kwa muda mrefu

  • Hipothemia ina uwezekano mkubwa wa kutokea ikiwa kuna hali ya upepo, uko kwenye maji ya baridi au umelowa, au huwezi kutembea tembea ili kupasha mwili joto

  • Mwanzo, hipothemia itakufanya utetemeke

  • Hipothemia inapozidi kuwa mbaya, unachanganyikiwa na kupoteza ufahamu

  • Watu wanaweza kufa ikiwa joto lao la mwili litapungua chini ya 88° F (kiasi cha 28° C)

  • Watoto wachanga na wazee ndio wenye hatari kubwa ya hipothemia

Onana na daktari mara moja ikiwa unahisi una hipothemia.

Je, nini husababisha hipothemia?

Hipothemia husababishwa na kukaa kwenye eneo lenye baridi na kushindwa kupasha joto mwili wako.

Una hatari kubwa ya kupata hipothemia ikiwa utakaa kwenye eneo lenye baridi na:

  • Husogezi mwili wako (kwa mfano, una majeraha au umepoteza ufahamu kutokana na kunywa pombe)

  • Una matatizo fulani ya kiafya, kama vile maambukizi, mzunguko mbaya wa damu au dundumio lisiloamilifu

  • Wewe ni mzee sana au mdogo sana

Si lazima iwe baridi sana. Unaweza kupata hipothemia hata wakati baridi ni sawa na 55 au 60° F (kiasi cha 13 to 16° C).

Zipi ni dalili za hipothemia?

Mwanzo unatetemeka sana na meno yako kutatarika

Hipothemia inapozidi kuwa mbaya, unaweza pia:

  • Kuwa mzito na goigoi

  • Kuchanganyikiwa na kujichelewa kuchukua hatua

  • Ukawa unachelewa kuchukua hatua

  • Ukapoteza uwezo wa kufanya maamuzi mazuri

  • Ukaanguka, kulala chini ili kupumzika au ukazurura

  • Kuacha kutetemeka na ukapoteza fahamu

Hatimaye, moyo wako utasimama (mshtuko wa moyo) na utaaga dunia. Hata hivyo, unahitaji oksijeni kidogo wakati unapokuwa na hali ya hipothemia. Baadhi ya watu wenye hali ya hipothemia, hasa watoto, wanaweza kuishi hadi kwa saa moja baada ya kupata mshtuko wa moyo.

Madaktari wanawezaje kujua ikiwa nina hipothemia?

Madaktari wanaweza kufahamu kuwa una hipothemia kwa kukagua joto lako. Iwapo joto lako ni chini ya 95° F (35° C), una hipothemia.

Je, madaktari wanatibu vipi hipothemia?

Mtu yeyote mwenye hali ya hipothemia anapaswa:

  • Kuvua nguo ambazo zimelowa na kuzikausha

  • Avae nguo nyingi zilizokauka, zenye joto pamoja na kofia na kujifunika kwa blangeti lenye joto

  • Kunywa kinywaji cha uvuguvugu

Ikiwa uko macho na unahisi baridi na kutetemeka, hatimaye hiki kitapasha joto mwili wako. Ikiwa unaonekana kuchanganyikiwa au goigoi, mtu anapaswa kukupeleka hospitalini. Huenda madaktari wakatakiwa kukupatia matibabu maalumu ya kuongeza joto.

Hospitalini, madaktari wanaweza kuongeza joto la mwili wako kwa kutumia njia zifuatazo:

  • Kukupa oksijeni ya joto kwa ajili ya kupumua

  • Kusukuma kiowevu cha uvuguvugu kwenye mishipa yako kupitia IV au kwenye tumbo lako kupitia bomba

  • Wakati mwingine, kupasha joto damu yako kupitia mashine inayovuta damu yako nje ya mwili wako, ikaipasha joto, na kuisukuma irudi mwilini mwako

Usifanye CPR (ufufuaji wa moyo na mapafu) kwa mtu ambaye amepata hipothemia, kwa sababu inaweza kuharibu moyo wake. Piga tu 911 ili mtu huyo aweze kuletwa hospitalini mara moja.

Ninawezaje kuzuia hipothemia?

Unaweza kuzuia hipothemia kwenye maeneo ya baridi kwa:

  • Kuvaa kofia

  • Kubaki ukiwa mkavu

  • Kwa kuwa na matabaka kadhaa ya nguo ambazo unavua au kuvaa ili kupata joto lakini sio kupata jasho na kulowa

Wazee ni rahisi kupata hipothemia, hivyo wanapaswa:

  • Kuhakikisha nyumba zao zina angalau halijoto ya 68° F (20° C), hasa chumbani

  • Kuvaa matabaka kadhaa ya nguo na kuhakikisha wanafunika kichwa na vidole vyao vya mikono na miguu wakati ambapo hali ya hewa ni ya baridi

  • Kuvaa nguo zilizoundwa kwa sufi na vifaa vingine vya kukuhami

  • Kula vyakula vya na vinywaji vya vuguvugu (lakini si pombe) wanapokuwa kwenye sehemu za baridi

  • Kutembea tembea wanapohisi baridi, ili kupasha joto mili yao

Ikiwa huwezi kuweka nyumba yako katika hali yenye joto la kutosha, tafuta mpango wa usaidizi wa nishati katika eneo lako ili kupata usaidizi wa gharama.