Ugonjwa wa Osgood-Schlatter

Imepitiwa/Imerekebishwa Sept 2023

Ugonjwa wa Osgood-Schlatter ni nini?

Ugonjwa wa Osgood-Schlatter ni uvimbe wenye maumivu makali ya mfupa na gegedu kwenye sehemu ya juu ya mguu wa chini wa mtoto (mfupa chini ya goti).

  • Osgood-Schlatter kwa kawaida hutokea kwa watoto wenye umri wa miaka 10 hadi 15 ambao wanashiriki katika michezo

  • Inasababishwa na mazoezi makali ya miguu

  • Mtoto wako atakuwa na maumivu, uvimbe, na uchungu kwenye goti moja

  • Madaktari hutibu ugonjwa wa Osgood-Schlatter kwa dawa za maumivu na kupumzika

Dalili za ugonjwa wa Osgood-Schlatter ni zipi?

Dalili za Osgood-Schlatter ni pamoja na:

  • Maumivu, uvimbe na uchungu mbele ya goti, chini kidogo ya pia ya goti

  • Maumivu ambayo yanazidi mazoezi yanapozidi na kupoa unapopumzika

Kwa kawaida dalili huwa kwenye goti moja tu.

Madaktari wanawezaje kujua kama mtoto wangu ana ugonjwa wa Osgood-Schlatter?

Madaktari wanaweza kujua kama mtoto wako ana Osgood-Schlatter kwa kuulizia dalili za mtoto wako na kumfanyia uchunguzi wa mwili. Wakati mwingine, madaktari hufanya eksirei.

Madaktari hutibu vipi ugonjwa wa Osgood-Schlatter?

Daktari ataelekeza mtoto wako:

  • Pumzika na uepuke kupiga magoti sana

  • Kumeza dawa za kutibu uvimbe (NSAIDS) zisizo za steroidi, kama vile ibuprofen

  • Fanya mazoezi ya kujinyoosha

  • Weka barafu juu ya goti

Kawaida watoto wanaweza kuendelea kucheza wakiendelea kupona. Kwa kawaida dalili hupotea baada ya wiki au miezi kadhaa.

Ikiwa hali ya ugonjwa imezidi, madaktari wanaweza:

  • Kuweka plasta kwenye mguu

  • Kumpa dozi za kotikosteroidi

  • Fanya upasuaji